Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatatu,Machi 29: Uhuru Aonywa na ODM Dhidi ya Kumsaliti Raila

A2aa84a07dfd1814 Magazeti Jumatatu,Machi 29: Uhuru Aonywa na ODM Dhidi ya Kumsaliti Raila

Tue, 30 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatatu, Machi 29, yameripoti kuwa sheria mpya iliyowekwa kuzuia msambao wa COVID-19 na Rais Uhuru Kenyatta Ijumaa, Machi 26, itaathiri rifarenda ya BBI.

Magazeti haya pia yameripotia kuhusu uchungu ambao sehemu ya Wakenya walikumbana nayo wikendi baada ya magari ya umma kupandisha nauli kufuatia marufuku ya kuingia na kutoka katika kaunti zilizoathirwa pakubwa na COVID-19.

1. People Daily Magari ya uchukuzi yameongeza nauli baada ya kaunti tano kufungwa.

Kulingana na gazeti hili, abiria wengi walipigania magari ya umma ili kuafikiana na makataa ya Jumapili, Machi 28, kufuatia Rais Uhuru kupiga marufuku shughuli za kuingia na kutoka katika kaunti tano.

Idadi jumla ya maambukizi ya COVID-19 nchni ilipanda kutoka 2% hadi 22% kati ya Januari na Machi huku Nairobi ikiongoza kwa 60% ya visa hivyo.

Uhuru alisema idadi ya waliolazwa hospitalini iliongezeka kwa 52% ndani ya wiki mbili na watu saba kufariki kila siku kutokana na virusi hivyo.

2. The Standard Gazeti hili limeangazia hatua ambazo serikali imepiga kupitia Wizara ya Afya kuwalinda wafanyakazi kwenye mstari wa mbele dhidi ya janga la kimataifa.

"Juhudi za kuwalinda wafanyakazi kwenye mstari wa mbele dhidi ya janga zimekumbwa na utata, dhana potovu na urongo. Lakini baada ya watu 90,000 kuchanjwa,Wakenya wametoa maoni yao," iliripoti gazeti hili

Wakenya wamehimizwa kuchanjwa dhidi ya COVID-19, serikali ikishikilia kuwa watu wanaojilinda pamoja na wenzao ndio wanachangia kupungua kwa makali ya janga hilo.

3. Daily Nation Daily Nation limeripoti namna Uhuru anakumbana na presha ya kulegeza masharti baada ya kuweka sheria mpya ya kuzuia msambao wa COVID-19.

Uhuru hakupunguza ushuru wakati wa kutoa masharti hayo na kuwaacha Wakenya na mzigo.

Kiongozi huyo alishikilia kuwa masharti hayo ni ya muda ili kuzuia kusambaa kwa ugonjwa huo na vifo licha ya athari kwenye uchumi.

Hakuna aina yoyote ya uchukuzi inaruhusiwa katika kaunti za Nairobi, Kajiado, Kiambu, Machakos, na Nakuru.

Sheria ya kafyu sasa ni kuanzia saa mbili usiku hadi saa nne asubuhi katika kaunti hizo tano.

4. Taifa Leo Wanasiasa wanaomuegemea kiongozi wa chama cha ODM, Raila Odinga wamemuonya Uhuru dhidi ya kumfungia kinara huyo nje ya BBI wakisema kuwa hatua hiyo itasambaratisha mipango yote na matunda kutokana na handisheki.

Wakiongozwa na Mbunge wa Ugunja Opiyo Wandayi, walisema njama yoyote ya kumsaliti Raila itashindwa.

Pia waliwataja watu ambao wanaongoza mipango ya kumaliza Raila kisiasa.

5. The Star Gazeti hili linaripoti kuhusu mpango wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kutoa mafunzo kwa makamishna na wakurugenzi. Zoezi hilo litagharimu mamilioni ya pesa.

Makamishna wa tume hiyo, Wafula Chebukati (mwenyekiti), Boya Molu, na Abdi Guliye, na maafisa wengine wanatazamaiwa kushiriki mafunzo hayo katika makundi mawili kuanzia Aprili 1 hadi Aprili 12.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke