Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatatu, Juni 21: Jinsi Ruto alinoa makali yake kisiasa kujiandaa 2022

1a4e30f8e86e8c8b Magazeti Jumatatu, Juni 21: Jinsi Ruto alinoa makali yake kisiasa kujiandaa 2022

Mon, 21 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatatu, Juni 21, yameripotia masuala kadhaa siasa zikipewa kipaumbele. Muungano wa kisiasa 2022 kati ya ODM na chama tawala Jubilee ndio taarifa kuu.

1. Daily Nation Gazeti hili limeangazia vizingiti vinavyokumba muungano wa kisiasa kati ya Jubilee na ODM ambao wakeketaji wanaamini utatumika katika Uchaguzi Mkuu wa 2022.

Huku ODM kikipania kufanya kazi pamoja na Jubilee, mrengo wa National Super Alliance (NASA) unakosoa hatua hiyo.

Inasemekana kuwa hakuna chama kinachoweza kubuni mrengo mwingine ilhali bado hakijavunja muungano ulipo.

ODM kinataka kuungana na Jubilee japo chama hicho cha upinzani hakijivunja makubaliano yake na NASA.

2. The StandardGazeti hili limeripotia namna Naibu Rais William Ruto ametengwa na serikali huku wadhifa wake ukinyakuliwa na kiongozi wa ODM, Raila Odinga.

Ruto amekosekana katika hafla kadhaa zilizoandaliwa Ikulu huku Raila akihudhuria karibia zote.

Ruto na Rais Uhuru Kenyatta wamekuwa wakipgana vita baridi huku wakikutana tu wakati wa hafla za kitaifa na mikutano ya baraza la mawaziri.

Wajibu wa Ruto ulikabidhiwa Waziri wa Usalama Fred Mariang'i, ambaye amegeuka kuwa msaidizi wa Uhuru.

Kutokana na mpasuko huo, wandani wa Ruto wamekuwa wakiadhibiwa baadhi wakipoteza nyadifa zao serikalini na bungeni.

3. People Daily People Daily imeangazia namna Ruto alibuni himaya yake akijiandaa kuhimarisha nafasi zake za kumrithi Uhuru.

Punde baada ya kushinda uchaguzi wa 2013, Ruto alianza kunoa makali yake kisiasa huku akijipatia utajiri wa kufadhili ndoto yake.

Kutoka kwa kupata cheo kubwa serikalini, kufanya ziara nchini, kukaguab miradi na hata kutembelea makanisa tofauti, Ruto aligeuka kuwa mtu mwenye ushawishi mkubwa kisiasa.

4. The StarKulingana na gazeti hili, vinara wa NASA wamepuzilia mbali mpango wa Jubilee kuungana na ODM kufanya kazi pamoja 2022.

Viongozi wa ANC na Wiper wamekosoa hatua hiyo ya chama chao tanzu ODM kuugana na chama kinachoongozwa na Rais Uhuru Kenyatta, Jubilee.

The Star linaripoti kuwa vyama hivyo vimekataa kuungana tena na ODM baada ya Uhuru kuwahimiza vinara hao kaungana pamoja na kumchagua mgombea atakayepambana na Naibu Rais William Ruto mwaka 2022.

5. Taifa Leo Taifa Leo linaripotia unafiki wa viongozi ambao wanakiuka sheria za kuzuia COVID na kisha kuwataka wananche kufuata kanuni hizo.

Kampeni za kisiasa zimekuwa zikifanyika na kuwaweka wananchi katika hatari ya kupata virusi hivyo.

Visa viliongezeka maradufu Kisumu baada ya sherehe ya Siku Kuu ya Madaraka mnamo Juni 1.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 073248269.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke