Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatatu, Juni 14: Ruto awatumia mawaziri kumfichulia siri za Uhuru

53a46bdd24fafabb Magazeti Jumatatu, Juni 14: Ruto awatumia mawaziri kumfichulia siri za Uhuru

Mon, 14 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatatu, Juni 14, yameangazia siasa zinazotokisa chama cha Jubilee.

Magazeti haya pia yameripotia siasa za sasa katika eneo la Mlima Kenya huku chaguzi za 2022 zikikaribia.

1. The Standard Gazeti hili limeripotia mpasuko katika Chama cha Jubilee chini ya miaka mitano tangu ya kubuniwa.

Chama hicho kilizinduliwa Septemba 2016 kufuatia vyama 11 vya kisiasa kuvunjwa na kuungana pamoja.

Baada ya kushinda uchaguzi wa urais mwaka 2017, Rais Uhuru Kenyatta amekuwa akitimiza kimya chake kuhusu masaibu ya chama hicho na kupelekea baadhi ya wanachama kugura na kutafuta hifadhi kwingine.

Chama hicho kinadaiwa kufa, bila ya uchaguzi rasmi miaka minne tangu kubuniwa kwake. Viongozi wa sekritariati wanashikilia nyadhifa za kaimu.

Wiki jana, naibu mwenyekiti wa chama hicho, David Murathe alifichua kuwa amechoshwa na cheo hicho akidai misheni yake imekwisha.

Murathe alisema kibarua chake kilikuwa kuwaadhibu waasi waliojiunga na chama cha United Democratic Alliance (UDA).

UDA kinachohusiana na Naibu Rais William Ruto, kinapigiwa debe kama chama ambacho Ruto atatumia kuwania urais katika uchaguzi ujao.

Gavana wa Kirinyaga, Anne Waiguru pia alikiri kwamba chama hicho kimekufa na ni kibarua kikubwa kukifufua.

Huku Uhuru akikaribia kustaafu, masuala yanayokumba chama cha Jubilee yanaonekana kutomzingua.

2. Daily Nation Daily Nation limeripotia mgawanyiko katika baraza la mawaziri la Uhuru ambalo lina wanachama wanaomuegemea Ruto ambaye anatofautiana na bosi wake.

Gazeti hili linaripoti kwamba mawaziri hao wanasubiri wakati muafaka kuwadia kabla ya kuanza kumuunga Ruto mkono hadharani kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2022.

Ruto anasemakana kufanya mkutano na mawaziri hao kupanga mikakati ya 2022.

Kutokana na hofu ya kunyanyaswa na washirika wa Uhuru, mikutano ya Ruto na mawaziri hao imekuwa ikifanyika kisiri.

Ruto pia amekiri kufanya mikutano hiyo ambayo alisema ilikuwa inalenga kuhimarisha mipango yake ya kufufua uchumi punde atakaposhinda urais.

Mawaziri hao wanaaminika kumfichulia Ruto siri za Uhuru.

3. Taifa Leo Kulingana na gazeti hili, kiongozi wa ANC Musalia Mudavadi amepuzilia mbali uwezekano wa kufufua muungano wa National Super Alliance (NASA) kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Hii ni baada ya kinara wa ODM, Raila Odinga kufichua kuwa huenda ataungana na mwenzake wa Wiper, Kalonzo Musyoka kupitia muungano huo wa 2017.

Katika uchaguzi wa mwaka wa 2017, Raila alipeperusha bendera ya NASA ambapo Kalonzo alikuwa mgombea mwenza, vinara wengine Mudavadi, Moses Wetangula na Isaac Rutto wakiwa na matumaini ya kushikilia nyadhifa kubwa endapo muungano huo ungelichukuwa hatamu za uongozi.

Akizungumza mjini Mombasa Jumapili, Juni 13, Mudavadi alisema Raila alishindwa kutimiza makubaliano ya awali na hivyo hawezi kuungana naye katika chaguzi za 2022.

4. The Star Gazeti hili limeguzi siasa za mgawanyiko katika eneo la Mlima Kenya ambalo hudaiwa kuwa na wapiga kura wengi.

Huku wanasiasa wa mashariki wakivutana na wa magharibi, The Star limeangazia jamii ambazo zitawateua viongozi wa kuwania nyadhifa kubwa serikalini.

Huenda Ruto na Raila Odinga watatumia mvutano huo kutimiza ajenda yao na kisiasa kushinda kiti cha urais.

Wale wa mashariki wametangaza kuwania kiti cha urais na hawataunga mkono wenzao wa magharibi ambao wametawala eneo hilo kwa miaka mingi.

"Kile mnatuonyesa wenzetu hatuwezi kuenda pamoja. Endapo ni kugawanyika, wacha tugawanyike kila mtu aende pekee yake," alisema Sente awa Meru Mithika Linturi.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke