Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatatu, Julai 5: Matiang'i anolewa kumenyana na Ruto 2022

6a80cb3e40454302 Magazeti Jumatatu, Julai 5: Matiang'i anolewa kumenyana na Ruto 2022

Mon, 5 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatatu, Julai 5, yameripotia kuhusu vita vya maneno kati ya Naibu wa Rais William Ruto na waziri mkuu wa zamani Raila Odinga.

Magazeti haya pia yameangazia uwezekano wa Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i kunolewa kukabiliana na Ruto katika kinyang'anyiro cha urais.

1. The StarKulingana na chapisho hili, huenda Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i atapendekezwa kumenyana na Ruto katika chaguzi za 2022.

The Star linaripoti kuwa Matiang'i anashirikiana na Raila kuunganisha eneo la Nyanza kumpigia kura.

Waziri huyo anadaiwa kuwa kifaa bora na pia anayependelewa sana katika baraza la mawaziri wa Rais Uhuru Kenyatta.

Anaaminika kuchukuwa wadhifa wa Ruto kwa kukagua miradi za Uhuru.

Kutokana na wajibu wake serikalini, Matiang'i anatambuliwa kama mmoja wa viongozi wakuu eneo la Nyanza na mwenye uwezo wa kukutanisha viongozi.

Hivyo anaonekana mgombea bora zaidi wa kumbwaga Ruto ambaye ana hamu ya kumrithi Uhuru.

2. Daily Nation Gazeti hili limeangazia kuhusu vita vya maneno kati ya Naibu wa Rais William Ruto na hasimu wake kisiasa Raila Odinga.

Wikendi, viongozi hao wawili walishambuliana kuhusu madai ya ufisadi.

Hii ni baada ya Raila kusema serikali yake itawaadhibu na kuwafunga viongozi fisadi.

Katika kumjibu, Ruto alisema Raila si msafi akimkashifu kushuhudia wizi wa mamilioni ya pesa katika sakata ya Kemsa na mpango wa Kazi Kwa Vijana ambao uliibuka wakati wa serikali ya muungano.

Raila alishangazwa na namna Ruto huwa na wasiwasi kila mjadala wa ufisadi ukitajwa bila jina lake kutajwa.

Kinara huyo wa ODM alimuhimiza Ruto ajiuzulu kwa sababu ya kuamua kupinga serikali.

3. People Daily People Daily pia iliangazia makabiliano ya Raila na Ruto kuhusu vita vya ufisadi.

Waziri mkuu huyo wa zamani alisema iwapo atamrithi Uhuru kama rais wa tano, serikali yake itaanza kuwaadhibu wanaohusishwa na kesi za ufisadi.

Matamshi ya Raila tyalioneknaa kumlenga Ruto ambaye alimsuta.

Ruto alisema upande wa Upinzani chini ya Raila uliongoza visa vya ufisadi na hivyo hana mamlaka ya kumfunza yeyote jinsi ya kukabiliana na ufisadi.

4. Taifa Leo Kulingana na gazeti hili, Raila atawania urais katika uchaguzi mkuu ujao.

Kinara huyo wa ODM anaripotiwa kuwa tayari ameanza kuwashawishi wapigakura wamchague.

Akizungumza mjini Mombasa wikendi iliyopita, Raila alisema ajenda yake kuu ni kufufua uchumi na kuwaadhibu wanaotuhumiwa na ufisadi.

Awali alisema kuwa atatangaza azma yake baada ya mchakato wa BBI kumalizika.

5. The Standard Gazeti hili linaripotia namna walimu wakuu wanatumia wazazi kujifaidi kwa kuwalipisha pesa kabla ya kuwapa wanao nafasi katika kidato cha kwanza.

Kulingana na The Standard, shule hizo huwalipisha wazazi kati ya KSh 5,000 na KSh 35,000 kwa madai ya "ada ya maendelee" ambazo bila kulipa wanafunzi hao watanyimwa barua.

Licha ya onyo kutoka kwa serikali, walimu wakuu wanadai kuwa ada hiyo iliidhinishwa na bodi ya shule na wazazi.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke