Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatatu, Aprili 5: Mudavadi na Ruto wampigania Raila

Df6f7da4ae045d71 Magazeti Jumatatu, Aprili 5: Mudavadi na Ruto wampigania Raila

Mon, 5 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatatu, Aprili 5, yameripotia kuhusu uwezekano wa kiongozi wa ODM Raila Odinga kuungana na Naibu Rais William Ruto katika Uchaguzi Mkuu wa 2022. One Kenya Alliance pia unalenga kutumia ushawishi wa Raila 2022.

Magazeti haya pia yamegusia pigo kubwa ambalo makanisa yalipata baada ya serikali kupiga marufuku mikutano ya hadhara huku polisi wakivuruga ibada katika baadhi ya makanisa kwa kukiuka sheria za COVID-19.

1. The Standard Gazeti hili limeangazia uwezekano wa muungano wa kisiasa ambao utabuniwa kabla ya uchaguzi wa 2022.

Baada ya uhasama kudhihirika kati yao, kiongozi wa chama cha Amani National (ANC) Musalia Mudavadi sasa amedokezea kufanya kazi na Raila Odinga huku uchaguzi mkuu wa 2022 ukikaribia.

Mudavadi alisema kuungana na Raila kutasaidia One Kenya Alliance kuleta sura mpya katika siasa za urithi za Rais Uhuru Kenyatta.

Gazeti hili limefichua kwamba kulikuwepo na njama ya serikali kumtenga Raila na kugusia uwezekano wa muungano wa kisiasa kati ya Ruto na Raila hatua ambayo haitawafurahisha wandani wa Ruto kutoka eneo la Mlima Kenya.

Wandani hao wanapinga muungano huo wakidai kwamba utakumbwa na usaliti na mchezo chafu.

2. Daily Nation Chapisho hili linaripotia namna makanisa yameathirika tangu masharti mapya ya COVID-19 kutolewa na Uhuru Ijumaa, Machi 26.

Makanisa katika kaunti za Nairobi, Kajiado, Kiambu, Nakuru na Machakos zilifungwa kwa muda.

Hata hivyo, makanisa mengine katika kaunti 42 zililazimika kupunguza idadi ya waumini.

Makanisa hayo yalisema yalikuwa yametumia pesa zote za ustawi kutoa michango kwa sababu ya kuongezeka kwa visa vya COVID-19 lakini sasa mpango huo umesitishwa.

Sherehe ya Pasaka iligeuka kuwa ya upweke baada ya serikali kupiga marufuku mikusanyiko na hivyo kuwa vigumu kwa waumini kukutana siku ya Ijumaa Kuu.

3. Taifa Leo Gazeti hili linaripotia kuhusu maafisa wa serikali ambao wameonyesha nia ya kuwania viti katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Miongoni mwao ni Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i, ambaye amependekezwa kuwania urais, msemaji wa polisi Charles Owino ambaye alitangaza atamrithi Cornel Rasanga kama gavana wa Siaya na Katibu Mkuu wa Usalama wa Ndani Karanja Kibicho, ambaye anadaiwa kuwa na nia ya kuwania ugavana Kirinyaga.

Mratibu wa eneo la Bonde la Ufa George Natembeya pia anasukumwa kuwania ugavana Trans Nzoia, waziri wa fedha Ukur Yattani, ambaye anaweza rejea Marsabit kupigania tena kiti chake cha ugavana.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke