Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatatu, Aprili 26: Viongozi wanaotamani kuwa naibu wa Ruto 2022

9b9f522093e168a5 Magazeti Jumatatu, Aprili 26: Viongozi wanaotamani kuwa naibu wa Ruto 2022

Mon, 26 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatatu, Aprili 26, yameripotia pakubwa kuhusu wanaomezea mate kiti cha Naibu Rais.

Magazeti haya pia yameguzia hali ya janga la COVID-19 nchini India, ambayo imeshuhudia taifa hilo likirekodi idadi kubwa ya maambukizi na vifo kila siku.

1. The Standard Gazeti hili linaripotia siasa za 2022 na kuwaguzia wagombea wanaoazimia kunyakuwa kiti cha naibu rais.

Huku wagombea wa urais wakijitokeza kwenye kivumbi, wale ambao wanatamani kuwa wagombea wenza pia wamejitokeza na kuweka mbinu ya kuwavizia wakubwa wao.

Viongozi wa Tangatanga kutoka eneo la Mlima Kenya wamefanya mikutano kadhaa kujadiliana jinsi Naibu Rais William Ruto atamteua mmoja wao kuwa mgombea mwenza.

Miongoni mwa wale ambao wana azimia kuwa naibu wa Ruto ni ikiwemo waziri wa zamani wa kilimo Mwangi Kiunjuri, kiongozi wa Narc Kenya Martha Karua, Mbunge wa Gatundu Kusini Moses Kuria, na gavana wa zamani wa Kiambu William Kabogo.

Wanaojipendekeza kwa kiongozi wa ODM Raila Odinga ni ikiwemo Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru, Gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya na wenzake wa Pwani, Hassan Joho(Mombasa) na Amason Kingi wa Kilifi.

2. Daily Nation Daily Nation limeripotia hali ya COVID-19 nchini India ambapo hospitali mjini New Delhi zimeanza kujaa pomoni huku visa vya maambukizi na vifo vikishtua ulimwengu.

Ndani ya saa 24, visa 349,691 vipya vimeripotiwa, wagonjwa 2,767 wakimalizwa na virusi hivyo.

Hata hivyo serikali imelaumiwa kwa kushindwa kujipanga kabla ya mlipuko huo licha ya dalili za mapema.

Waziri mkuu Narendra Modi alitaja janga hilo kama dhoruba linaloyumbisha taifa, akiwaomba wananchi kuchanjwa na kujiepusha na fununu zinazosambazwa kuhusu ugonjwa huo.

Baadhi ya majimbo ya taifa hilo, ikiwemo Delhi, yameweka marufuku ya kuingia na kutoka ili kupunguza kueneza kwa ugonjwa huo.

3. People DailyGazeti hili pia limeguzia siasa za 2022 na kuweka uzito kwa wagombeaji wanaopania kuchukuwa kiti cha naibu rais.

Huku eneo la Mlima Kenya likiongoza, wanasiasa wa eneo hilo wanataka kuendelea kuwa na kiti chenye mamlaka kubwa baada ya kutawala miaka minne tangu uhuru.

Viongozi wa Tangatanga kutoka eneo hilo walitangaza kusimama na Ruto.

Hata hivyo, wanamtaka achague mgombea mwenza kutoka eneo hilo katika uchaguzi mkuu ujao.

Raila Odinga, kwa upande wake pia anaandamwa na wanasiasa wengi ambao tayari wameonyesa nia ya kumuunga mkono kuinga Ikulu.

4. The Star Kwenye gazeti hili Seneta wa Busia Amos Wako, amezungumzia maisha yake baada ya kunaswa na COVID-19.

Baada ya kipindi hicho, Wako alisema alitambua kuwa utajiri na mamlaka si mambo ya maana.

Alisema alijua kwamba hataondoka hospitalini akiwa hai na tayari alikuwa amejiandaa kukumbana na mauti.

Alikuwa na vitabu vitatu vya kiroho kando yake ambavyo alikuwa anavisoma akijiandaa kufa.

Baada ya kushinda vita dhidi ya virusi hivyo, Wako, ambaye ni mwanasheria mkuu wa zamani alisema aliangalia maisha yake na kubadilisha mawazo yake.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke