Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatatu, Agosti 23: AG kupinga uamuzi wa BBI katika Mahakama ya Juu

E0369b46d10a266a Magazeti Jumatatu, Agosti 23: AG kupinga uamuzi wa BBI katika Mahakama ya Juu

Mon, 23 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatatu, Agosti 23, yameripotia kuhusu mwelekeo wa Mpango wa Maridhiano (BBI) kufuatia uamuzi wa Mahakama ya Rufaa wa kuuharamisha.

Magazeti haya pia yameguzia mashambulizi ya Naibu Rais William Ruto dhidi ya wakereketwa wa mswada huo.

1. Daily NationKulingana na gazeti hili, wabunge wanaomuegemea Rais Uhuru Kenyata watazindua majaribio yao ya kufufua reggae ya BBI kupitia Bunge la Kitaifa.

Wabunge hao wanadaiwa kuchukuwa vipengee 52 kutoka kwa mswada huo, wakidai vinaweza kubadilishwa bila kuhusisha umma.

Wanapania kupitisha mapendekezo hayo kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Mapendekezo hayo ambayo wabunge watashinikiza ni:

Kuongeza maeneo bunge kutoka 290 hadi 360 Kulinda maeneo bunge 26 ambayo hayakuafikia kanuni za idadi ya watu mwaka 2012 Uteuzi wa wagombeaji wa urais na wagombea wenza wao kupitia Bunge baada ya Uchaguzi mkuu Wabunge waliochaguliwa kuapishwa kuwa mawaziri Kuongeza pesa zinazotengewa kaunti kuwa angalu 35% ya ugavi wa mapato Kubuniwa kwa Hazina ya Maendelo ya Wadi kuchukuwa 5% ya bajeti ya maendeleo ya bunge Vijana kutolipa ushuru kwa miaka saba kwa kubuni tume ya vijana

Read also

Hatimaye Raila Atangaza Rasmi Atawania Kiti cha Urais 2022

2. The StandardNaibu Rais anaendelea kuwashambulia wakereketwa wa BBI ambao aliwataja kama wabinafsi.

Ruto, ambaye mashambulizi yalionekana kumlenga rais na kiongozi wa ODM Raila Odinga, aliwashtumu kutumia BBI kujinufaisha binafsi.

Kulingana naye ni Mungu ndiye alisitisha mchakato huo wa kubadilisha katiba kwa sababu hakufurahishwa nao na hivyo aliamua kwa faida ya Wakenya.

"Ni kwa mpango wa Mungu kuwa tumshirikishe kila mmoja kwa masuala hayo. Haiwezekani kama wengine hawatashirikishwa," alisema.

Kufuatia kuzikwa kwa BBI, Ruto aliwataka wandani wa handisheki kumruhusu rais kutekeleza ajenda yake akijiandaa kuondoka madarakani.

3. People DailyKulingana na gazeti hili, Mwanasheria Mkuu Kihara Kariuki atawasilisha kesi katika Mahakama ya Upeo kukosoa uamuzi wa Mahakama ya Rufaa mnamo Agosti 20 wa kushikilia uamuzi wa Mahakama Kuu kuwa BBI ni haramu.

Huku wakikataa mswada huo, majaji hao walisema rais hana mamlaka ya kushinikiza Katiba kufanyiwa mabadiliko na anaweza kushtakiwa.

Kariuki alipinga zogo hilo akiapa kupambana na majaji hao katika Mahakama ya Upeo.



Read also

Aisha Jumwa Awasisimua Wakenya na Densi ya Kishua Baada ya BBI kuzimwa

Katika stakabadhi, Kariuki alitaja vigezo vitano ambavyo atavitumia kuwasilisha rufaa yake katika Mahakam ya Upeo.

Hii ni ikiwemo muundo msingi wa mswada huo, kuondoa marekebisho ya katiba na mpango maarufu wa kumlinda rais.

Kuhusu muundo msingi wa mswada huo, Kariuki alihoji kuwa majaji wa Mahakama ya Rufaa na Mahakama Kuu walivuka mipaka ya mamlaka yao katika uamuzi wao.

Kariuki pia alikosoa majaji kwa kumtaja Uhuru kama mkereketwa wa BBI ambayo ilikuwa inalenga kubadilisha katiba.

4. Taifa Leo Taifa Leo linaripoti kuwa Raila atasuka mbinu mpya ya 2022 baada ya Mahakama ya Rufaa kutupa nje BBI.

Chama cha ODM kinasemekana kupanga kikao cha wabunge wa chama hicho ambapo mikakati mapya yatapangwa.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke