Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatatu, Agosti 16: Raila aumwa kichwa kumchagua mgombea mwenza 2022

D1de27429df16542 Magazeti Jumatatu, Agosti 16: Raila aumwa kichwa kumchagua mgombea mwenza 2022

Mon, 16 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatatu, Agosti 16, yameipa uzito uamuzi unaosubiriwa kutolewa kuhusu kesi ya rufaa ya Mpango wa Maridhiano (BBI) iliyosikizwa na Mahakama ya Rufaa Juni 2021.

Magazeti haya pia yameguzia tandabelua inayomkumba kiongozi wa Orange Democratic Movement (ODM) Raila Odinga ya kumchagua mgombea mwenza wa uchaguzi wa urais ujao.

1. People Daily Baadaye wiki hii, jopo la majaji wa Mahakama ya Rufaa linaloongozwa na Daniel Musinga litatoa uamuzi kuhusu kesi ya rufaa ya BBI iliyosikizwa Juni.

Musinga alikuwa amesema jopo hilo litahitaji muda wa kupitia stakabathi kadha zilizowasilishwa na upande wote.

Zikiwa zimesalia siku nne kabla ya uamuzi huo kutolewa, wakereketwa wa BBI wana imani kuwa uamuzi huo utatolewa kwa faida yao, wakiongezea kuwa watatumia mbinu nyingine iwapo mahakama itashikilia uamuzi uliotoewa na Mahakama Kuu Mei 13.

Walalamishi walikosoa uamuzi huo katika mahakama ya rufaa.

Naibu Rais William Ruto, na washirika wake walifurahia uamuzi huo.



Hata hivyo, atapata pigo kisiasa iwapo Mahakama ya Rufaa itabatilisha uamuzi huo na kushikilia kuwa mswada huo ni halali kisheria.

Wakereketwa wa BBI wana nafasi ya kuelekea katika Mahakama ya Upeo iwapo uamuzi utatolewa dhidi yao.

2. The Standard Gazeti hili linaripotia siasa zinazochezewa na wandani wa vigogo wa siasa kujifaidi binafsi.

Hivi majuzi, wanasiasa hao wamekuwa wakirushiana cheche za maneno wakishikilia kuwa viongozi wao ndio bora kuwania urais mwaka ujao.

Seneta wa Kakamega, Cleophas Malala amekuwa akishikilia kuwa kiongozi wa ANC, Musalia Mudavadi hatamuunga mkono mgombea mwingine 2022.

Wandani wa kinara wa ODM, Raila Odinga, Kalonzo Musyoka wa Wiper na kiongozi wa KANU, Gideon Moi pia wamesisitiza kuwa viongozi wao hawatazima ndoto zao kuwaunga mkono wagombea wengine.

Wengi wa wanasiasa hao wanalenga kuchaguliwa tena na wengine wakimezea mate vyeo vikubwa mwaka ujao na hivyo ni lazima wawe karibu na vigogo wakuu wa siasa.

Kwa mfano Malala anamezea mate kiti cha ugavana Kakamega, wachanguzi wakidai anataka kutumia umaarufu wa Mudavadi kushinda kiti hicho.

Hali hiyo ni sawia katika kambi ya Ruto ambapo wandani wake wanatumia umaarufu wake kushinda viti mwakani.

3. The Star The Star linaripotia namna kinara wa ODM yuko njia kipanda kuhusu kumchagua mgombea wa urais mwaka 2022.

Licha ya kutotangaza rasmi azma yake, Raila amedhihirisha kuwa atakabiliana na Ruto kwenye kivumbi hicho.

Kwa sasa anafurahia urafiki wake na Rais Uhuru Kenyatta, ambao umekuwepo tangu mwaka 2018.

Kibarua kigumu cha Raila ni kumchagua mgombea mwenza ambaye atamsaidia kutwaa ushindi katika uchaguzi wa urais.

Uhuru amekuwa akiwashinikiza vinara wa NASA kuungana ambao wameanza kampeni zao za kuingia Ikulu mwakani.

Kiongozi wa Wiper, Kalonzo amekuwa mgombea mwenza wa Raila kwa muda.

Hata hivyo, alisema haweza tena kumuunga mkono Raila baada ya kukataa kutimiza ahadi yake ambayo iliunda mrengo wa NASA katika chaguzi za awali.

Fauka ya hayo, Raila yuko huru kumchagua mgombea mwenza kutoka Mlima Kenya katika dhamira ya kuwavizia wakazi wa eneo hilo lenye wapiga kua wengi.



4. Daily Nation Kulingana na Daily Nation, mafuta ni bei rahisi Nakuru kuliko Nairobi.

Licha ya Nakuru kuwa kilomita chache kutoka Nairobi, watumizi wanashangaa iweje bidhaa hiyo ni bei rahisi badala ya Nairobi.

Kwa mfano jijini Nairobi, lita moja ya mafuta ya petroli ni KSh 127.14 huku Nakuru ikuuzwa KSh 126.75.

Katika mfumo wa kawaida, bei ya mafuta huwa ghali ukisafiri kutokea Mombasa kwa sababu ya ada ya usafirishaji.

5. Taifa Leo Gazeti hili limeangazia wimbi mpya wa siasa unaopiga eneo la Mlima Kenya huku waniaji wakuu kwenye kinyang'anyiro cha urais wakipigania kura.

Kwa sasa eneo hilo limegawanyika huku upande mmoja ukimuunga mkono Ruto, na mwingine Raila.

Hata hivyo, kuna sehemu ya wakazi ambao wameshikilia kuwa eneo hilo litakuwa na wakilishi wao.

Wiki jana, Charity Ngilu, Moses Kuria na Mwangi Kiunjuri walikutana pamoja kuunda timu ambayo itamrithi Uhuru, ambaye muhula wake utatamatika 2022.

Watatu hao waliapa kushirikiana kufufua makali ya Mt Kenya katika siasa za taifa hili.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke