Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatano: Tajiri Jimmy Wanjigi akera ODM kwa kumuita Raila mzee

0d45a35f1913369e Uamuzi kesi ya ugaidi dhidi ya Mbowe leo

Wed, 1 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatano yameangazia suala la walinzi wa Naibu Rais William Ruto ambapo wiki jana wandani wake waliteta kuhusu maafisa wa GSU kuondolewa katika makao yake Karen na Sugoi.

Aidha kuna mgogoro ambao unaibuka katika chama cha ODM baada ya tajiri Jimmy Wanjigi kutangaza kuwania urais kwa tiketi ya chama hicho.

The Star

Jarida hili linaripoti kuwa wandani wa Raila Odinga wamekerwa na tajiri Jimmy Wanjigi na kampeni zake za kuingia Ikulu kupitia tiketi ya ODM.

Wanjigi amekuwa akimtaka Raila kuondoka kuachana na urais 2022 na kukipa kizazi kipya nafasi ya kuwania urais.

Wandani wa Raila wanasema matamshi ya Wanjigi huenda yakaeneza dhana kuwa Raila ni mzee na anafaa kuondoka.

Aidha katibu Edwin Sifuna na mwenyekiti John Mbadi walisema Wanjigi amefungua afisi mbadala za chama na hivyo kuzua maswali kuhusu mpango wake.

People Daily

Taarifa katika gazeti la People Daily ni kuhusu hatua ya kamati ya bunge kumuita Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i kuelezea kuhusu usalama wa naibu rais William Ruto.

Hii ni baada ya kundolewa kwa maafisa wa GSU kutoka ulinzi wa makao ya DP Karen na kijijini Sugoi.

Ruto hata hivyo amekuwa akiwataka wabunge kutomhoji Matiang'i akisema hana shida na kuondolewa kwa maafisa hao.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke