Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatano: Raila Akutana na Matajiri wa Mlima Kupanga 2022

B815c8cbb0d2a557 Magazeti Jumatano: Raila Akutana na Matajiri wa Mlima Kupanga 2022

Wed, 29 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatano Septemba 29 yameendelea kuangazia juhudi za kinara wa ODM Raila Odinga kutafuta uungwaji mkono na eneo la Mt Kenya kwenye safari yake ya kuingia Ikulu 2022.

1. People Daily

Siku moja tu baada ya kinara wa ODM kufanya ziara katika eneo la Mt Kenya na kuhubiri ajenda yake kwa eneo hilo, sasa amefanya kikao na wafanyabiashara sugu kutoka Mlima.

Raila alikuwa katika mkahawa wa Safari Park ambapo alikutana na mabwanyenye hao wakiongozwa na mwenyekiti wa benki ya Equity Peter Munga.

Chini ya mwavuli wa Mt Kenya Foundation, Raila alipata nafasi ya kuuza sera zake kwa kikao hicho.

Baadhi ya wanachama wa vuguvugu hilo ni mjomba wake Rais Uhuru Kenyatta, George Muhoho, SK Macharia wa RMS, mkurugenzi wa KenGen Eddy Njoroge na wengine.

2. Star

Gazeti hili pia linaangazia siasa za 2022 ambapo naibu rais William Ruto na kinara wa ODM Raila Odinga wanajikakamua kucheza kadi zao.

Jarida hili linasema DP Ruto anaonekana kubadili mwelekeo wa siasa zake na sasa ameachana na ajenda ya hustlers vs dynasties.

Aidha inaarifiwa kuwa ametafuta kundi lingine na washauri ili kumsaidia kukwea Mlima wa kuingia Ikulu 2022.

3. Nation

Gazeti la Nation lina taarifa kuhusu kurejea kwa aliyekuwa mkurugenzi wa tume huru ya mipaka na uchaguzi nchini IEBC Ezra Chiloba.

Chiloba sasa ameteuliwa kujiunga na tume ya mawisiliano nchini CAK kama mkurugenzi.

4. Standard

Gazeti la Standard linasema Rais Uhuru Kneyatta amewapa wanachama wa Mt Kenya Foundation wajibu wa kumtafuta kigogo atakayeungwa mkono na eneo la Mt Kneya katika uchaguzi wa urais 2022.

Kundi hilo liliketi na Raila Odinga Jumanne Septemba 28 na sasa inaarifiwa Kalonzo Musyoka, Musalia Mudavadi na Gideon Moi pamoja na Moses Wetangula watahudhuria kikao chao Ijumaa Sepetmba 30.

Naibu Rais William Hata hivyo ametengwa na wanasema hawatamuita kuuza sera zake.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke