Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatano: ODM Watoa Ishara ya Kumsaliti Rais Uhuru Kwenye BBI

6536c6b0eef594e4 Magazeti Jumatano: ODM Watoa Ishara ya Kumsaliti Rais Uhuru Kwenye BBI

Wed, 31 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatano yameangazia taarifa kadhaa zikiwamo za usalaama wa Naibu Rais William Ruto baada ya taarifa kuwa drone ilipepea juu ya anga ya nyumba yake Karen.

Kuna taarifa za siasa kuhusu mageuzi ya kikatiba yanayotarajiwa kupitia BBI huku wandani wa kinara wa ODM Raila Odinga wakionekana kubadili mkondo.

1. Standard

Katibu wa ODM Edwin Sifuna aliitaka serikali kutumia fedha zozote zilizokuwa zimetengewa mchakato wa BBI kusaidia Wakenya kukabiliana na janga la coronavirus.

Akiongea kwenye mahojiano na runinga ya Citizen Jumanne Machi 30, Sifuna alisema fedha kama hizo zinafaa kutumika kununua chanjo ya kukabilia Covid-19.

Matamshi ya Sifuna yamechukuliwa kwa uzito na mhariri wa Standard anasema huenda kuna njama ya kusambaratisha mkondo wa BBI ambao ODM imekuwa ikiunga mkono pakubwa.

Mhariri pia ameangazia mtihani wa kitaifa unaoendelea huku kukiwa na uvumi kuwa baadhi ya shule zinahusika katika udanganyifu.

2. People Daily

Taarifa kuhusiana na raia wa kigeni aliyepeprusha drone yake mpaka kwenye anga za nyumba ya DP Ruto mtaani Karen zimepakiwa kwenye gazeti hili huku mwandishi akizua maswali kuhusu tukio hilo.

Raia huyo alikamatwa baada ya mkewe DP, Rachael Ruto kuripoti kisa hicho kwa maafisa wa polisi Jumatatu Machi 29.

Kuna taarifa pia kuhusu maziko ya Mama Sarah Obama aliyezikwa Jumanne Machi 30 siku moja baada ya kifo chake.

Alikuwa ni maarufu kutokana na mjukuu wake Barrack Obama kuwahi kuwa rais wa nchi yenye nguvu duniani, Marekani.

3. Star

Gazeti la Star ni kuhusiana na sakata ya KEMSA ambapo walipa ushuru walipoteza mabilioni kwenye ununuzi wa vifaa vya kukabiliana na coronavirus.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke