Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatano: Mt Kenya yawakazia Ruto na Raila, watakiwa kutoboka zaidi

1d578b993da17731 Magazeti Jumatano: Mt Kenya yawakazia Ruto na Raila, watakiwa kutoboka zaidi

Wed, 22 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti yameangazia taarifa kuhusu vile eneo la Mt Kenya linajipanga kuhakikisha linapata nafasi kwenye serikali ijayo.

Kuna taarifa pia kuhusu wabunge kuskiza kilio cha Wakenya kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta.

1. Star Kenya

Taarifa kwenye gazeti hili ni kuhusu juhudi zinazoendelea za kuleta viongozi wa Mt Kenya pamoja ili kutetea maslahi ya jamii yao wakiwa pamoja.

Kulingana na ripoti hii, vigogo katika eneo la Mt Kenya wanataka wagombea wa urais wanaovuma kuwa na makubaliano na wao kuhusu watakachopata wakiwaunga mkono.

Duru zimearifu kuwa eneo hilo linataka MoU na naibu rais William Ruto au Raila Odinga iwapo wanataka kuungwa mkono.

People Daily

Gazeti hili limeangazia umoja wa wabunge kutetea bei za mafuta wakisema Wakenya wengi wanaumia kutokana na kuongezwa na bei ya kila lita ya petroli, mafuta taa na diseli.

Spika wa bunge Justin Muturi alisema njia mufti ya kukabili suala la bei za mafuta ni kuwe na sheria inayolinda bei hizo.

Kamati ya kawi bungeni ilipewa siku 14 kuunda mswada utakaoidhinishwa na kuwa sheria ili kuwalinda Wakenya dhidi ya gharama kubwa za mafuta.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke