Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatano, Mei 5: Kiatu cha Raila chazua mpasuko ODM

C51047a5e13efd2f Magazeti Jumatano, Mei 5: Kiatu cha Raila chazua mpasuko ODM

Wed, 5 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatano, Mei 5, yameripotia ziara ya siku mbili ya Rais wa Tanzania Samia Suluhu nchini Kenya kama kiongozi wa taifa.

Magazeti haya pia yameangazia mgawanyiko mkubwa unaokumba chama kinachoongozwa na Raila Odinga, ODM huku makundi kadhaa yakibuniwa kumrithi kigogo huyo.

1. Daily Nation Kulingana na Daily Nation, Chama cha Jubilee kimekataa kufanya mazungumzo na chama kinachohusishwa na Naibu Rais William Ruto, United Democratic Alliance (UDA).

Naibu mwenyekiti wa Jubilee, David Murathe alisema uamuzi wa kuvunja maafikiano kati ya chama tawala na UDA ambacho awali kilijulikana kama Party of Development and Reforms (PDF) hauwezi kubadilika.

Hata hivyo, Murathe alisema endapo viongozi wa UDA watajiepusha na kukiuka sheria za maadili ya Jubilee, basi chama hicho kinachoongozwa na Rais Uhuru Kenyatta kitasitisha mpango wa kuwaadhibu.

Pia aliwaonya wabunge wa Tangatanga dhidi ya kusitisha mchango wa kila mwezi wa Jubilee akisema watakuwa wamevunja sheria za chama.

2. Taifa Leo Katika gazeti hili, mvutano wa kumrithi Raila Odinga unatishia mpasuko katika chama cha Orange Democratic Movement (ODM).

Makundi kadhaa yanaibuka kutoka ODM; moja linaoongozwa na wabunge kama vile Junet Mohammed na John Mbadi, na lingine la Seneta wa Siaya James Orengo na la tatu linaongozwa na Gavana wa Migori Zachary Obado.

Kikosi cha Junet kinapania kuwaondoa wanasiasa wa muda mrefu kama vile Seneta wa Siaya.

Makundi yote yako na ari ya kuvalia kiatu cha Raila endapo atastaafu siasa mwaka 2022.

Raila bado hajazima mawimbi hayo katika chama chake lakini mkutano wa hivi majuzi kati yake na Mbunge wa Suna Mashariki unaonyesha kuwa anafahamu mgawanyiko unaokokota.

3. The Standard Gazeti hili limeangazia ziara ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu nchini kama kiongozi wa taifa.

Suluhu alilakiwa katika Ikulu ya Nairobi na Rais Uhuru Kenyatta kwa ziara yake ya siku mbili ambayo ilizima mkwaruzano kati ya mataifa hayo mawili.

Viongozi hao wawili walishuhudia kutiwa saini kwa makubaliano ya kujenga bomba ya gesi kati ya Dar es Salaam na Mombasa na kukubali kushirikiana katika masuala ya utamaduni, miundo msingi na usalama.

Hii leo Jumatano, Aprili 5, Suluhu atahutubia kikao cha pamoja cha Bunge mwendo wa saa nane unusu mchana.

4. The StarNaibu Rais William Ruto ameahidi kuzindua nembo ya ‘hustlers’ Disemba 2021, The Star limeripoti.

Ruto alionyesha matumaini kuwa ndoto yake ya kubadilisha Kenya itatimia akiapa kuwadhibitishia wakosoaji wake kuwa ana uwezo wa kuwajenga Wakenya.

Alisema ana imani kuwa mbinu yake ya uchumi itafaulu na pia itawafaidi Wakenya.

5. People DailyKulingana na People Daily, Waziri wa Uchukuzi James Macharia ameonya magari ya umma dhidi ya kuwabeba abiria kupita kiasi.

Macharia alisema taifa hili bado linakumbana na hatari ya COVID-19 na hivyo matatu yanatakiwa kufuata masharti ya kuzuia msambao.

Alisema masharti hayo yatalegezwa punde makali yakifika 2.5%.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke