Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatano, Mei 26: Uhuru amtaka Raila kubuni mrengo wa kumuadhibu Ruto

6c684b89e89aa266 Magazeti Jumatano, Mei 26: Uhuru amtaka Raila kubuni mrengo wa kumuadhibu Ruto

Wed, 26 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatano, Mei 26, yameipa uzito joto la kisiasa hususan Chama cha Jubilee na United Democratic Alliance (UDA) vinapojiandaa kumenyana kwenye uchaguzi mdogo wa Kiambaa.

Magazeti haya pia yameripotia kuhusu juhudi za kinara wa Upinzani Raila Odinga kuziba nyufa katika chama chake akijaribu kumsaka Gavana wa Mombasa Hassan Joho na mwenzke wa Kwale Salim Mvurya ili kuanza kupiga kampeni za kisiasa.

1. Daily NationKulingana na gazeti hili, Rais Uhuru Kenyatta amemuomba mwenzake wa handisheki Raila Odinga, kujadiliana na vinara wa One Kenya Alliance kubuni mrengo ambao utapambana na Naibu Rais William Ruto katika chaguzi za 2022.

Uhuru alimuomba kiongozi huyo wa ODM kufanya mkutano wa faragha na vigogo hao ambao tayari umeanza kujiandaa kwa Uchaguzi Mkuu.

Kinara huyo wa Upinzani pia anafanya mazungumzo na Gavana wa Mombasa Hassan Joho kuanza kupiga kampeni katika ukanda wa Pwani ambao umegawanyika zaidi.

Kufikia sasa mwandani wa Raila, mwanabiashara Edwin Ng'ong'o anaripotiwa kufanya mazungumzo na mwenyekiti wa KANU Gideon Moi kuzungumzia uwezekano wa kupanua mrengo wao.

2. Taifa LeoTaifa Leo linaripoti kuwa dawa za kupunguza makali ya Ukimwi (ARVs) ambazo zimekwama katika bandari ya Mombasa kwa miezi kadhaa zinakaribia kuharibika huku mzozo ukitokota kati ya Wizara ya Afya na USAID.

Ripoti zinadai kwamba dawa hizo zitaharibika endapo zitakosa kusambazwa kufikia Septemba mwaka huu.

Chanzo cha mzozo huo ni mfumo wa usambazaji ambapo USAID inapinga pendekezo la Wizara ya Afya ya kutumia Mamlaka ya kusambaza dawa nchini (KEMSA) kusambaza dawa hizo katika hospitali za kaunti.

Dawa hizo zinatajwa kuwekwa kwa muda wa miezi 18 hadi 24 kabla ya kuharibika na hivyo zinatakiwa zipelekewe wagonwa wa Ukimwi haraka ili ziwasaidie.

3. The Standard Uchaguzi mdogo wa Julai 15, 2021, wa Kiambaa kwa mara nyingine tena unatoa nafasi ya Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto kupambana.

The Standard linaripoti kuwa hii ni baada ya mgombea wa Chama cha Jubilee Karanja Kariri Njama na John Njuguna Wanjiku wa United Democratic Alliance (UDA) kuwasilisha stakabathi zao za uteuzi kwa IEBC Jumanne, Mei 25.

Uchaguzi huo unatoa nafasi kwa Uhuru kujaribu kunoa makali yake eneo la Mlima Kenya baada ya kupoteza katika uchaguzi mdogo wa Juja.

Wakati huo huo, Ruto kupitia mgombea wa UDA anapania kuhimarisha umaarufu wake katika ngome ya Uhuru baada ya kushinda chaguzi ndogo za Rurii na Juja.

4. People Daily Kulingana na People Daily, Kiongozi wa Wengi katika Bunge la Taifa Amos Kimunya ametetea hatua ya serikali kuchukuwa mikopo akisema ni muhimu katika kuhimarisha utoaji wa huduma.

Kimunya alipuzilia mbali madai kuwa hali ya sasa ya mkopo ni hatari akisema serikali ya Jubilee bado iko imara kwani pesa hizo zinatumika vyema.

Alisema kuna miradi nyingi ambazo zimefadhiliwa na mkopo huo akiongezea kuwa taifa hili linatakiwa kuwa na usawa katika ya mgao wa mapato na matumizi.

5. The Star Kulingana na The Star, maelfu ya Wakenya ambao walipoteza uraia wao chini ya katiba ya zamani watapata katika kipindi cha miezi miwili zijazo.

Hata hivyo, watalazimika kutuma maombi katika Jumba la Nyayo jijini Nairobi ama ubalozi nchini Kenya.

Kufika sasa zaidi ya maombi 25,000 yametumwa katika idara ya uhamiaji.

Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang’i amemwandikia mkuu wa sheria barua akimtaka kurahisisha utaratibu huo.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke