Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatano, Mei 19: Tangatanga wakanusha njama ya kumtimua Uhuru ofisini

7945c9393c9d8f62 Magazeti Jumatano, Mei 19: Tangatanga wakanusha njama ya kumtimua Uhuru ofisini

Wed, 19 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatano, Mei 19, yameripotia pakubwa kuhusu chaguzi ndogo za maeneo bunge ya Juja na Bonchari na wadi ya Rurii ambazo zilikuwa za amani lakini kuzingirwa na vioja.

Magazeti haya pia yameguzia kuhusu wandani wa naibu Rais William Ruto kubadilisha msimamo wao wa kumuondoa Rais Uhuru Kenyatta mamlakani baada ya kupatwa na hatia ya kuvunja sheria kufuatia uamuzi dhidi ya BBI.

1. The Standard Kulingana na The Standard, Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i amekuwa akitumia chaguzi ndogo ya eneo bunge la Bonchari kupima umaarufu wake katika jamii ya Gusii akijiandaa kwa 2022.

Japo waziri huyo hajatangaza wazi azma yake ya kuwania urais, baadhi ya mawaziri wenzake wamekuwa wakimpendekeza na hivyo ametumia chaguzi hiyo kama ngazi ya kupanda kisiasa.

Imeripotiwa kuwa Chama cha Jubilee hakitamteua mgombea wa uchaguzi huo lakini hatua ya dakika za mwisho ya Matiang'i ilimshuhduia Zedekiah Opore akiwekwa debeni na tikiti ya Jubilee.

Washirika wa Matiang'i walifichua kuwa waziri huyo ambaye anapedelewa sana na Rais Uhuru Kenyatta alikuwa anatumia chaguzi hiyo kujipima nguvu.

Hata hivyo, mgombea wa ODM Pavel Oimeke ndiye aliibuka mshindi na kura 8,049 huku Opore akiibuka wa pili na kura 7, 279.

2. Daily Nation Gazeti hili linaripoti kuwa wandani wa naibu Rais William Ruto wamepuzilia mbali madai kuwa watatumia uamuzi wa Alhamisi, Mei 13, dhidi ya BBI kama msingi wa kumuondoa Rais Uhuru Kenyatta mamlakani.

Hii ni baada ya wakili Charles Njama kusema mbunge yeyote ambaye angelipenda kumvua rais mamlaka afanye hivyo baada ya Mahakama Kuu kuamua kuwa Uhuru alivunja sheria kwa kuzindua mswada wa Mpango wa Maridhiano.

Wakiongozwa na mbunge wa Mathira Rigathi Gachagua, lengo la mrengo wa Tangatanga ni Uchaguzi Mkuu wa 2022 na watamruhusu rais akamilishe muhula wake na amani.

Mbunge wa Belgut Nelson Koech alikariri matamshi hayo akisema kumvua mamlaka kiongozi wa taifa haijawahi kuwa mpango wao.

3. Taifa Leo Kwenye Taifa Leo, imeibuka kuwa Rais Uhuru Kenyatta alimuokoa Gavana wa Bungoma Wycliffe Wangamati dhidi ya kufukuzwa mamlakani.

Hii ni baada ya wandani 45 wa Bunge la Kaunti hiyo kuwasilisha hoja ya kumtimua kwa msingi ya matumizi mabaya ya mamlaka na pesa za COVID-19.

Kiongozi wa wachache Francis Chemion aliagizwa kutupilia mbali hoja hiyo wakati wa mkutano kama amri kutoka Jubilee.

Wandani hao walisema walilazimika kufuata amri hiyo kutoka kwa Uhuru binafsi na kisha walikutana na gavana huyo kuzika tofauti zao.

4. The Star Wanajeshi kadhaa wa Jeshi la Ulinzi wa Kenya (KDF) wanahofiwa kufariki baada ya gari lao la kupiga doria kukanyaga bomu katika eneo la Baure, Lamu Mashariki.

Kundi la IED linashukiwa kutimiwa na wanamgambo wa al Shabaab ambao wamejificha katika Msitu wa Boni kutekeleza kitendo hicho cha Jumanne, Mei 18.

Kamishna wa polisi kaunti ya Lamu Irungu Macharia alisema idadi kamili ya majeruhi haijulikani kwani eneo hilo lina changamoto ya mawasiliano.

5. People DailyKatika gazeti hili, Bunge la Kitaifa hii leo Jumatano, mei 19, litafanya mkutano maalum wa kuamua hatma ya jaji mkuu mteule Martha Koome.

Kwenye taarifa iliyochapishwa kwenye gazeti rasmi la serikali, Spika Justin Muturi aliwaomba wabunge kuhudhuria kikao hicho.

Kiongozi wa wengi Amos Kimunya alithibitisha kuwa wabunge watakutana leo kuidhinisha ama kupinga uteuzi wa Koome.

Mnamo Alhamisi, Mei 13, Kamati ya Bunge kuhusu Sheria na Masuala ya Kikatiba kubaini ilimpiga msasa kuhusu ufaafu wake kwa wadhifa huo.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke