Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatano, Agosti 4: Misheni ya ziara ya DP Ruto Uganda yafichuliwa

651e7001488690e5 Magazeti ya Kenya leo August 4, 2021

Wed, 4 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatano, Agosti 4, yameripotia pakubwa kuhusu kuzuiwa kwa Naibu Rais William Ruto kusafiri Uganda huku ikibanika alitakiwa kukutana na washirika wa Rais Museveni kupewa ushauri.

1. The StarKulingana na gazeti hili maafisa wakuu serikalini wamefichua kuwa Naibu Rais William Ruto hataruhusiwa kuondoka nchini bila kupewa ruhusa na Rais Uhuru Kenyatta.

Maafisa hao ambao majina yao yalibanwa walisema sheria hizo mpya zilitolewa wiki mbili zilizopita baada ya ziara ya Ruto nchini Zanzibar.

Afisa moja alisema kuwa mabalozi pia wamepewa masharti makali ya kutopanga ziara za Ruto bila kuidhinishwa na rais kupitia barua.

Haya yanajiri baada ya Ruto kuzuiwa kusafiri hadi Uganda Jumatatu, Agosti 2.

2. Daily Nation Katika gazeti hili, Naibu Rais William Ruto alikuwa anatazamiwa kusafiri hadi Uganda kufanya mazungumzo na washauri wa Rais Yoweri Museveni akijiandaa kuwania urais 2022.

Kulingana na wandani wa Ruto, naibu rais alikuwa anatazamiwa kufanya mazungumzo ya faragha na Museveni huku wandani wake wakijadiliana na maafisa wa chama cha National Resistance Movement (NRM).

Read also

Magazeti Jumanne, Agosti 3: Sababu ya Ruto Kuzuiwa Kutangatanga Uganda

Mbunge wa Kapseret, Oscar Sudi, alisema Ruto anamtafuta mshauri wa siasa ambaye anatumainia kumpata kupitia Musevani kufuatia na kukwaruzana na Rais Uhuru Kenyatta.

Sudi alisema japo Ruto alizuiwa kusafiri hadi Uganda, wandani wake waliopewa kibali walifanya mazungumzo na washirika wa Museveni.

3. Taifa Leo Katika gazeti hili, vinara wa muungani wa One Kenya Alliance wamemomb mwenyekiti wa Kanu Gideon Moi kutalikiana na Rais Uhuru Kenyatta kwa kuvunja ushirikiano na chama cha Jubilee.

Katika mkutano mtaani Karen, Nairobi ambao seneta huyo wa Baringo alikosa kuhudhiria, Kiongozi wa Ford Kenya, Moses Wetang'ula, Musalia Mudavadi (ANC) na Kalonzo Musyoka (Wiper) walisema Moi anatakiwa kuvunja mkataba huto wa maelewani hataka iwezekany.

Hata hivyo Katibu Mkuu wa Kanu, Nick Salat, alisema kuwa chama hicho hakiko tayari kujiunga na OKA kwani kingali na mkataba wa ushirikiano na Jubilee.

Wakati wa mkutan huo wa Karen, watatu hao walitangaza kuvunjwa kwa muungano wa NASA uliobuniwa kabla ya uchaguzi mkuu wa 2017 pamoja na kiongozi wa ODM Raila Odinga.



Read also

DP Ruto Azungumza Baada ya Serikali Kumzuia Kusafiri Uganda "Namwachia Mungu"

4. The Standard Katika gazeti la The Standard, Seneta wa Baringo Gideon Moi ameonyesha matumaini kuwa uamuzi wa Mahahama Kuu kuharamisha BBI utabatilishwa.

Moi alisema BBI ina manufaa mengi kwa Wakenya ikiwemo kufufua uchumi hususan wakati huu wa janga la COVID-19 linalokeketa nchi.

Pia alisem BBI itasaidia uwepo na mawakilishi wengi na hivyo kuleta maendeleo.

Jopo la majaji saba linatazamiwa kutoa uamuzi wa kesi ya rufaa Agosti 20.

5. People DailyWatalaam wa afya wamewaonya Wakenya kujiandaa kwa kuongezeka kwa maambukizi ya COVID-19 katika kipindi cha miezi miwili ijayo, People Daily linaripoti.

Kulingana na watalaam hao, hali hiyo itachochewa na aina mpya ya virusi hivyo vya Deltra.

Naibu mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Kimatibabu Kenya(KEMRI) Matilu Mwao alisema virusi hivyo vimeenea karibia nchi mzima akiongezea kuwa Wakenya wanatakiwa kuchanjwa na kufuata sheria za Wizara ya Afya kuzuia msambao.

Alisema virusi hivyo vitasalia kwa miezi mitatu kabla ya aina nyingine kulipuka kulingana na idadi ya watu watakaoambukizwa.



Read also

Magazeti Ijumaa, Julai 30: Sababu za ODM Kujiondoa NASA Zatajwa

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke