Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumanne, Septemba 14: Raila atumia mashamba kuvizia jamii ya Maasai

70046cfdd5c7f322 Magazeti Jumanne, Septemba 14: Raila atumia mashamba kuvizia jamii ya Maasai

Tue, 14 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumanne, Septemba 14, yameipa uzito hatua ya kiongozi wa Chama cha Orange Democratic Movement (ODM) Raila Odinga kuvizia jamii ya Maasai kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2022.

Magazeti haya pia yameripotia mipango ya Chama cha KANU kumtambulisha mpeperushaji wa bendera yake Septemba atakayekabiliana na Naibu Rais William Ruto.

1. Daily Nation Mnamo Jumatatu, Septemba 13, Raila alikutana na wajumbe kutoka Kajiado, Narok, Samburu na Laikipia katika eneo la Ongata Rongai, akiahidi kulinda haki zao za ardhi iwapo atachaguliwa kuwa rais 2022.

Waziri mkuu huyo wa zamani aliahidi jamii hiyo kuwa suala la mzozo wa ardhi litasalia kuwa historia.

Raila alisema iwapo mswada wa Mpango wa Maridhiano utapitishwa, pesa zinazotengewa kaunti ya Kajiado zitaongezwa hadi KSh 12.8 bilioni.

Kwa upande mwingine, mgao wa kaunti ya Narok utaongezeka kwa KSh 5 bilioni kutoka kwa sasa KSh 8 bilioni hadi KSh 13 bilioni.

2. The Standard



Kulingana na The Standard, itakuwa vigumu kwa Mahakama ya Kimataifa kuhusu Uhalifu (ICC), kuwafuatilia mashahidi ambao hawazungumzi lugha ya kitaifa ya Kenya.

Hii ni baada ya msajali kutaka upande wa mashtaka na utetezi kuwaagiza mashahidi kuzungumza tu Kingereza au Kiswahili.

Wakati huo huo, msajili alisema kuwa amri hiyo itawalinda mashahidi dhidi ya hatari iliyoripotiwa kwake.

Jaji Miatta Maria Samba alikubali ombi la wakili Mkenya Paul Gicheru na masharti kuwa hatachelewesha vikao vya mahakama.

3. Taifa Leo Gazeti hili linaripoti kuwa viongozi kutoka jamii ya Samburu wanaitaka serikali kumfichua mmiliki wa ardhi ya ADC Laikipia Mutara Ranch katika kaunti ya Laikipia.

Shamba hilo la ekari 15,000 awali lilihusishwa na Naibu Rais William Ruto.

Viogozi hao sasa wanataka kipande hicho cha ardhi kigawanye kwa jamii baada ya Ruto kukana kuwa si mmiliki mnamo Alhamisi, Septemba 9, wakati wa mkutano na wajumbe wa jamii ya Maasai.



Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang’i, Jumatano, Septemba 1, alianika mali na biashara zinazomilikiwa na Ruto na kulindwa na serikali.

4. People Daily Katika gazeti hili, wabunge wanaowaegema Rais Uhuru Kenyatta na Raila wanapanga mpango mpya wa kubuni nyadhifa za waziri mkuu, naibu wawili na makamu wa rais wawili.

Katika mpango huo, wabunge hao wanachama wa Kamati ya Kitaifa kuhusu Utekelezaji wa Katiba wanapanga washa Mombasa mnamo Jumanne wiki ijayo kubuni mswada wa kupendekeza vyeo hivyo vipya ambavyo vitashinikiza taifa kuandaa rifarenda pamoja na Uchaguzi Mkuu wa Agosti 9, 2022.

Njama yao ni moja ya juhudi mpya kuokoa mswada wa BBI ambao uliharamishwa na Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa.

Wale ambao watafaidika ni wanasiasa kadhaa ambao wametangaza azma ya kuwania urais.

5. The Star Ubabe unajikokota kati ya Ruto na kinara wa KANU, Gideon Moi kufuatia madai kuwa Gideon atajiunga na mbio za kuwania urais 2022.



Ruto ndio amekuwa mfalme wa siasa Bonde la Ufa akimtwaa rais wa zamani Daniel Moi, hata hivyo, Gideon anapania kurejesha taji hilo.

The Star limetambua kuwa Gideon, ambaye ni hasidi mkubwa wa Ruto, tayari ameanza mikakati ya kuchapisha manifesto yake
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke