Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumanne, Novemba 2: Jubilee kufukuza wanachama waasi kwa faida ya Raila

0b5f432bf0113283 Magazeti Jumanne, Novemba 2: Jubilee kufukuza wanachama waasi kwa faida ya Raila

Tue, 2 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumanne, Novemba 2, yameripotia pakubwa kuhusu,mipango ya Jubilee kuwatupa nje wanachama waasi na kuhimarisha muungano wake na chama cha Orange Democratic Movement (ODM).

Magazeti haya pia yanaripotia kuwa Mahakama Kuu mjini Eldoret imerefusha muda kwa wiki moja zoezi la kuwasajili wapiga ambalo lilikuwa linatazamiwa kukamilika leo.

1. Daily Nation Chama kinachoongozwa na Rais Uhuru Kenyatta, Jubilee kitaandaa Kongamano la Kitaifa la Wajumbe wa chama hicho (NDC) mwishoni mwa mwezi.

Wakati wa hafla hiyo, mpasuko wa kisiasa kati ya Uhuru na naibu wake William Ruto unatarajiwa kujitokeza.

Kufuatia mpasuko huo, kinara wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM), Raila Odinga atatambulishwa na Jubilee kama mshirika mpya.

Kamati ya Kitaifa ya Usimamizi wa chama hicho pamoja na uongozi wa bunge zinatazamiwa kuwapokonya wanachama watundu nyadhifa zao.

2. Taifa Leo Mahakama ya Rufaa imesitisha kwa muda amri ya Mahakama Kuu ya kumtaka Uhuru kuwaapisha majaji sita ambao alikuwa amewakataa.

Majaji Roselyn Nambuye, Imaana Laibuta na Wanjiru Karanja walipiga breki amri hiyo hadi Novemba 19, wakati watatoa uamuzi huo kuhusu iwapo watazuia Mahakama Kuu kushikiniza sita hao kuapishwa au la.

Majaji hao walifikia uamuzi huo baada ya kusikiliza malalamishi ya Mwanasheria Mkuu, Uhuru na taasisi ya Katiba kuhusu uteuzi wa majaji hao sita.

Pia waliangazia rufaa mbili iliyowasilishwa na Uhuru na Mwanasheria Mmuu kukosoa uamuzi wa Mahakama Kuu.

3. The Standard Ruto na baadhi ya washirika wake wa United Democratic Alliance (UDA) wamepuzilia mbali uamuzi wa Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang’i kuunga mkono Raila kuwania urais.

Wakihutubia wakazi katika barabara ya Sotik-Keroka Jumatatu, Novemba 1, Ruto aliongoza mashambulizi hayo pamoja na Mbunge wa Mwala Vincent Kawaya, wabunge wa Gusii na wanasiasa wengine.

Ruto alionyesha matumaini kuwa ataunda serikali mpya.

Alimtupia vijembe Raila, na vinara wa One Kenya Alliance (OKA) ambao alisema hawana mipango yoyote kwa taifa hili.

4. People DailyMahakama Kuu mjini Eldoret imerefusha muda kwa wiki moja zoezi la kuwasajili wapiga ambalo lilikuwa linatazamiwa kukamilika leo.

Jaji Eric Ogolla alizuia Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka(IEBC) kufunga zoezi hilo hadi kesi iliyowasilishwa na Patrick Cherono itakaposikizwa na kuamuliwa Alhamisi ijayo.

IEBC mnamo Oktoba 4, wakati ilikuwa ikizindua zoezi hilo ilisema ilikuwa inalenga kuwasajili wapiga kura wapya milioni sita ndani ya wiki nne.

Lakini taarifa kutoka kwa mwenyekiti wa tume hiyo Wafula Chebukati inaonyesha kuwa watu 800,462 pekee ndio walikuwa wamejisajili kufikia wiki ya tatu.

5. The Star Katika gazeti hili, mwanaharakati wa kutetea mazingira nchini Kenya, Elizabeth Wathuti amewataka viongozi ulimwenguni kuchukuwa hatua za haraka za kupambana na tabia nchi.

Akizungumza kando ya Kongamano la Umoja wa Mataifa kuhusu Tabia Nchi siku ya Jumatatu,Novemba 1, Wathuti, 26, aliwakumbusha viongozi ulimwenguni kuwa watoto na vijana wanasubiri hatua yao.

Aliwaambia viongozi wa duniani kuwa milioni ya Wakenya wanakumbana na hatari za tabia nchi kama vile baa la njaa sababu ya serikali zote duniani kushindwa kupata suluhu.

Hotuba yake ilikujia kabla ya Uhuru, kuongoza viongozi wa Afrika katika kutafuta suluhu katika kongamano hilo la tabia nchi.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke