Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumanne, Aprili 13: Matumaini makali ya COVID-19 ikipungua nchini

A456a96207d9968d Magazeti Jumanne, Aprili 13: Matumaini makali ya COVID-19 ikipungua nchini

Tue, 13 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumanne, Aprili 13, yameripotia pakubwa kuhusu kubuniwa kwa mirengo ya kisiasa ikiwa imesalia miezi 16 pekee Uchaguzi Mkuu kuandaliwa.

Magazeti haya pia yameripotia kuhusu kupungua kwa maambukizi ya COVID-19 ambayo inatoa matumaini kuwa maisha ya kawaida karibu kuanzan kurejea

1. Daily Nation Kulingana na gazeti hili, kuna matumaini ya hali kurejea kawaida na masharti ya COVID-19 kulegezwa baada ya wataalam kutangaza kuwa kizingo cha virusi hivyo vimeanza kupungua.

Kaimu mkurugenzi mkuu wa afya, Patrick Amoth alisema serikali inafuatilia msambao wa COVID-19 akiongezea kuwa washikadau watamshauri vyema endapo ugonjwa huo utapungua kusambaa ndani ya siku 14.

Amoth alisema idadi ya maambukizi imekuwa ikipungua tangu Rais Uhuru Kenyatta kuweka marufuku ya kuingia na kutoka maeneo kadhaa, kufungwa kwa makanisa na baa Machi 26.

2. Taifa Leo Gazeti hili linaangazia mchezo ambao vigogo wa kisiasa wanachezeana huku chaguzi za mwaka 2022 zikikaribia.

Mwanzo Rais Uhuru Kenyatta amekuwa akiegemea mrengo wa One Kenya Alliance ambapo wachanganuzi wanasema kutamchochea kiongozi wa ODM Raila Odinga kufanya mazungumzo ya kuungana na naibu Rais William Ruto.

Duru ilifichua kuwa Uhuru alimpigia Raila simu baada ya kuibuka kuwa Gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya alikutana na Ruto Jumatano, Aprili 7.

Wachanganuzi wa siasa walibaini kwamba kuna njama ya kuwalemaza Raila na wanasiasa wakuu wa Magharibi na Pwani ili kuwashinikiza kuunga mkono One Kenya Alliance.

3. The Standard Kulingana na The Standard, zoezi la chanjo ya COVID-19 litaendelea bila kutatizwa kwa sababu hakuna thibitisho ya kisa cha kuganda kwa damu kutokana na chanjo ya AstraZeneca.

Ahmed Kalebi, ambaye ni mwanapatholojia alisema chini ya watu 50 wameripotiwa kuwa na tatizo la kuganda damu Kenya ikilinganishwa na mataifa mengine ulimwenguni.

Daktari huyo alisema kuganda damu husababishwa na mambo mengi kama vile chakula na maisha ya kila siku.

Alisema endapo Kenya itakosa chanjo ya kutosha ya AstraZeneca, chanjo zingine zitatengenezwa kukinga virusi hivyo.

4. People Daily Kulingana na People Daily, Seneta wa Siaya James Orengo amesuta muungano wa One Kenya Alliance akishikilia kuwa Wakenya hawatalazimishwa kuwapigia wanasiasa fulani kura.

Alisema muungano huo ambao uliwaleta pamoja kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka, kiongozi wa Ford Kenya, Moses Wetang'ula, Musalia Mudavadi wa Amani National Congress na Gideon Moi wa KANU hauwezi kuwashawishi Wakenya kuwa utaboresha taifa.

Orengo alisema Wakenya ndio wataamua wakati wa chaguzi za 2022 na wala sio watu wachache serikalini.

5. The StarKwenye The Star, mabunge mapya 70 yaliyopendekezwa na Mpango wa Maridhiano (BBI) hayatajumuishwa kwenye chaguzi za 2022 endapo rifarenda haitaandaliwa kabla ya Agosti 8, 2021.

Haya yanajiri kukiwa na wasiwasi kuhusu rifarenda ya BBI itachelewa kutokana na kesi nyingi kortini dhidi ya mchakato huo.

Hii inamaanisha kwamba Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) itashindwa kuafikia mahitaji ya katiba.

Kwa mapendekezo hayo kutekelezwa katika uchaguzi ujao, basi mabunge hayo yanatakiwa kubuniwa kabla ya Agosti 8, 2021, miezi 12 kabla ya Uchaguzi Mkuu.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke