Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumanne, Agosti 3: Ruto hakumuomba Uhuru kibali kusafiri Uganda

4903fa5ba0094b09 Magazeti ya Kenya leo

Tue, 3 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumanne, Agosti 3, yameipa uzito tukio la Naibu Rais William Ruto kuzuiwa kusafiri hadi nchi jirani ya Uganda kwa ziara ya kibinafsi baada ya kusimamishwa na maafisa wa uhamiaji katika Uwanja wa Ndege wa Wilson Airport na kumuagiza kutafuta kibali ya serikali.

Magazeti haya pia yameripotia kuhusu idadi kubwa ya wanafunzi waliojitokeza kujiunga na Kidato cha Kwanza huku walimu wakuu wakilalamikia msongamano kutokana na sheria ya 100%.

1. The StandardGazeti hili linaripoti kuhusu mipango ya chama cha Orange Democratic Movement (ODM) kuungana na vyama vingine vya kisiasa kubuni mrengo wa kukabiliana na Ruto katika Uchaguzi Mkuu wa 2022.

Kiongozi wa ODM ametangaza mipango ya misururu ya mikutano kote nchini kuanzia Ijumaa, Agosti 6, kujadili njia mwafaka.

Raila alisema ana uwezo wa kutosha kuzoa kura zote nchini.



Read also

DP Ruto Azungumza Baada ya Serikali Kumzuia Kusafiri Uganda "Namwachia Mungu"

Waziri mkuu huyo wa zamani pia ameapa kuongeza umaarufu wake katika eneo la Mlima Kenya ambapo alipata kura chache wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2017.

2. Daily Nation Kulingana na gazeti hili, ofisi ya Ruto imekashifu vikali katika kile ilitaja kama kubadilishwa kwa sheria za kusimamia ziara zake tangu awe naibu wa rais mwaka 2013.

Maafisa wa uhamiaji walimzuia Ruto kusafiri hadi Entebbe, Uganda, akitokea Uwanja wa Ndege wa Wilson, Nairobi mchana wa Jumatatu, Agosti 2.

Katika ujumbe mfupi Jumatatu jioni, Ruto alionekana kusikitishwa na tukio hilo.

Maafisa wakuu wa usalama waliambia Daily Nation kuwa Ruto hakupewa kibali na bosi wake, Rais Uhuru Kenyatta kusafiri nje ya nchi kulingana na itifaki.

3. Taifa Leo Chapisho hili linaripotia kwamba wavuvi Wakenya katika eneo la Pwani wamezua malalamishi kuwa wanasukumwa nje na meli za kigeni.

Wavuvi hao wenye hamaki walisema meli za kigeni huvua samaji zote na kuwaacha mikono mitupu.



Read also

Aliyekuwa Naibu Gavana Jonathan Mueke Apanda Wheelbarrow, Ajiunga na Hustler ya DP Ruto

Taifa Leo pia linaripoti kuwa Mbunge wa Kimilili Didmus Barasa aliachiliwa huru kwa dhamana ya KSh 100,000 baada ya kukana shtaka la kumshambulia mkandarasi Stephen Masinde, almaarufu Steve Kay.

Barasa ambaye ni mwandani wa karibu wa Ruto, alikana shtaka la kumsababishia Steve madhara ya mwili kinyume na kifungu nambari 234 cha kanuni ya adhabu.

4. The Star Kulingana na The Star, wanafunzi 1,171,265 walioteuliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza katia shule mbali mbali wanatarajiwa kuanza kuripoti Jumatatu, Agosti 2, hasi Ijumaa, Agosti 6.

Kulikuwa na idadi kubwa ya wanafunzi waliojitokeza siku ya kwanza ya zoezi hilo.

Walimu wakuu wakilalamikia msongamano kutokana na sheria ya 100%.

Waziri Msaidizi wa Elimu Sarah Ruto alisimamia shughuli hiyo katika kaunti za Nairobi na Kiambu na kupongeza idadi ya waliojitokeza akisema mpango wa serikali kuhakikisha wanafunzi wote wanajiunga na shule za upili unaendelea vyema.

5. People DailyWabunge wa Bunge la Kitaifa watarejelea vikao vyao hii leo baada ya likizo fupi.



Read also

Magazeti Alhamisi, Julai 29: Wabunge Kupitisha BBI Bila Rifarenda

Miswada kadhaa zinatazamiwa kujadiliwa huku Mswada wa Kubadilisha Katiba 2020 ukipewa kipaumbele.

Marekebisho hayo yanapendekeza rais kuwatea mawaziri miongoni wa wabunge.

Hata hivyo, mswada huo utapata kizingiti baada ya mwanaharakati Okiya Omtatah kufika kortini akitaka mswada huo usijadiliwe akisema ni kinyume cha katiba.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke