Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumanne, Agosti 10: Rifarenda kufanywa uchaguzi ukiahirishwa, Maraga

D3997fe82175846e Magazeti Jumanne, Agosti 10: Rifarenda kufanywa uchaguzi ukiahirishwa, Maraga

Tue, 10 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumanne, Agosti 10, yameripotia pakubwa kuhusu pendekezo la Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) la kuwataka wanasiasa kutumia viwango vya juu vya pesa kwenye kampeni zao za Uchaguzi Mkuu wa 2022.

Magazeti haya pia yameguzia Naibu Rais William Ruto kushtumu vikali serikali ya Jubilee kwa kumkamata na kumtesa raia wa Uturuki Aydin Harun.

1. Daily Nation Kulingana na gazeti hili, bajeti ya KSh 40 bilioni ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) na matumizi ya pesa za kampeni ikiwemo KSh 4.4 bilioni za mwaniaji wa urais zimezua chaguzi ghali nchini.

Mnamo Jumatatu, Agosti 9, IEBC ilisema bado ina upungufu wa KSh 14.57 bilioni kwani Hazina ya Taifa iliitengea KSh 26.34 bilioni pekee za kuandaa Uchaguzi Mkuu wa 2022.

IEBC ilitetea bajeti ya KSh 40.9 bilioni ikitaja bei ghali ya karatasi za kura ambazo zinahitajika kuafikiana na vigezo tisa za usalama na maadili.



Read also

Wagonjwa Wengine 1,335 Wakutwa na Covid-19 Huku Wengine 30 Wakipoteza Maisha

Matumizi ya pesa za vyama vya kisiasa, viwango ambavyo vinahitajika ni KSh 17.7 bilioni, huku mahitaji mengine kama usafiri (KSh 11.8 bilioni), matangazo (KSh 1.8 bilioni), maajenti (KSh 11.5 bilioni).

2. The Standard Ikiwa imesalia mwaka mmoja uchaguzi mkuu kuandaliwa, IEBC imetangaza kuwa wafanyakazi wote wa serikali ambao wanataka kuwania viti vyovyote katika chaguzi za 2022, wanatakiwa kujiuzulu miezi sita kabla ya uchaguzi huo.

Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati alisema Mahakama ya Rufaa mjini Nyeri ilishikilia uamuzi wa Mahakama Kuu ya Kericho ambayo iliwapa wafanyakazi hao muda zaidi ofisini.

Chebukati aliongeza kuwa IEBC haitakubali orodha ya uteuzi ya vyama vya kisiasa ambayo haitatimiza sheria ya thuluthi tatu ya usawa wa jinsia.

Afisa Mkuu Mtendaji wa IEBC, Marjan Hussein alisema kuwa katika uchaguzi ujao, wanalenga kuwasajili wapiga kura 25 milioni kutoka kwa idadi ya sasa ya wapiga kura 20 milioni.

3. Taifa LeoKiongozi wa chama cha Wiper Democratic Movement, Kalonzo Musyoka amezindua kampeni zake za urais za mwaka 2022.



Read also

Magazeti Jumanne, Agosti 3: Sababu ya Ruto Kuzuiwa Kutangatanga Uganda

Makamu wa rais wa zamani Jumatatu, Agosti, 9, alizindua sera zake chini ya vigezo vitano vya uchumi.

Kalonzo alionyesha imani yake kuwa muungano wa One Kenya Alliance (OKA) utasalia imara wakati wa uchaguzi huo.

Kiongozi wa Amani National Congress (ANC), Musalia Mudavadi ambaye alikuwa miongoni mwa wageni waliohudhuria hafla hiyo alisema wataendelea kufanya kazi pamoja kama wanachama wa OKA kwa manufaa ya taifa hili.

4. The StarNaibu Rais William Ruto amewasuta maafisa wa serikali katika ofisi ya Rais akisema ndio walisababisha kukamatwa kwa Mturuki Aydin Harun kwa madai ya uwongo kwamba anahusika na ugaidi.

Katika kile kilioneka kumwelekezea Rais Uhuru Kenyatta kidole cha lawama, Ruto alisema alimpigia simu Aydin na kumuomba msamaha kwa niaba ya serikali kutokana na alichopitia.

Naibu Rais alisema Aydin aliteswa baada ya kukamatwa akitajwa kama "gaidi" lakini baadaye alitimuliwa nchini kama njia moja ya kuficha aibu.

Wakenya walishtuka Jumatatu, Agosti 9, asubuhi kufahimsihwa kwamba Aydin alitimuliwa nchini.

5. People Daily Huku taifa likijiandaa kwa uchaguzi mkuu ujao, aliyekuwa jaji mkuu David Maraga amepinga shinikizo la kutaka chaguzi hizo ziahirishwe.

Maraga alihoji kuwa kuahirishwa kwa uchaguzi huo utarefusha muhula wa Uhuru ofisini na hivyo rifarenda itahitajika kufanywa.

Maraga, ambaye aliongoza jopo la majaji wa Mahakama ya Upeo ambao walifuta matokeo ya uchaguzi wa urais mwaka 2017, amepinga hatua hiyo akisema hamna la msingi ambalo litahitaji tarehe ya uchaguzi kubadilishwa.

Viongozi wa upinzani Musalia Mudavadi, Kalonzo Musyoka na Martha Karua pia wamepinga mipango yoyote ya kutaka kuahirisha Uchaguzi Mkuu wa 2022.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke