Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Ijumaa: Umaarufu wa DP Ruto Mt Kenya sasa waanza kuyeyuka

E038771bdc2a86fe Magazeti Ijumaa: Umaarufu wa DP Ruto Mt Kenya sasa waanza kuyeyuka

Fri, 15 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Ijumaa yameangazia taarifa kadha ikiwamo ubabe wa kisiasa kati ya naibu rais William Ruto na kinara wa ODM Raila Odinga eneo la Mt Kenya.

Kuna taarifa pia kuhusu mauaji ya mwanariadha Agnes Tirop ambaye alipatikana amedungwa kisu katika kile kinaaminika kuwa mzozo wa kimapenzi.

1. Star

Star imefanya utafiti kuhusu ni mgombea yupi wa urais aliye maarufu katika eneo la Mt Kenya katika safari ya 2022.

Utafiti huo unaonyesha DP Ruto angali ana wafuasi wengi eneo hilo baada ya asilimia 57 ya waliohojiwa kusema wanamuunga mkono.

Asilimia 11 ndio walisema wako nyuma ya Baba na uchaguzi ukiitishwa leo watampa kura zao katika debe la iurais.

Hata hivyo, utafiti huo unaonyesha umaarufu wa DP unashuka tangu Raila aanze kampeni katika eneo hilo.

2. People Daily

Taarifas kuu hapa ni kuhusu Raila Odinga ambaye anaonekana kupata nguvu mpya katika safari ya kuelekea Ikulu.

Raila ameanza mikakati mipya ikiwamo kukutana na washikadau muhimu katika kutafuta kura za kutosha kumtangaza rais 2022.

Aidha ni wazi sasa kuwa serikali iko nyuma ya Raila jambo ambalo linampa nguvu ya kuvuma kisiasa.

Kuna taarifa pia kuhusu kutupwa nje kwa kadi ya Huduma na mahakama ikisema sheria haikufuatwa.

Serikali ilitumia mabilioni ya fedha katika kuwasajili Wakenya lakini korti ilisema hakuna sheria ya kulinda deta za watu.

3. Standard

Familia ya mwanariadha Agnes tirop inaendelea kuomboleza kifo chake huku mamake akisema binti huyo aliwatembelea siku tatu zilizopita kabla ya kupatikana ameuawa.

"Tulikuwa nyumbani Jumapili Oktoba 10 na kisha akaondoka ili kuanza mazoezi yake kule Iten. Alikuwa ameleta karo ya ndugu zake watano kwa sababu shule zinafunguliwa," mamake alisema.

Ametaka mkono wa serikali kuhakikisha kuwa familia yake inapata haki kwa kuwajibisha waliohusika.

"Nataka kujua ni kwa nini akamuua msichana ambaye amesaidia watu wengi hivi," mamake alisema.

Tayari makachero wa DCI wamemtia mbaroni mumewe ambaye anadaiwa alihusika katika mauaji hayo.

4. Nation

Jarida hili limezamia taarifa za mauaji ya Tirop ikiibuka mumewe alikuwa akimpa kichapo kwa mujibu wa dadake.

Kulingana na dadake, Tirop waligombana na mumewe siku ambaye alirejea nchini kutoka Tokyo na ilikuwa wazi kuwa ndoa yao ilikuwa na masaibu.

Aidha, licha ya mwili wake kupatikana Jumatano Oktoba 13, polisi wanachunguza iwapo huenda aliuawa Jumatatu usiku.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke