Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Ijumaa: Rais Uhuru na DP Ruto walitumiana jumbe za makasiriko

Ec94141d169d1c46 Magazeti Ijumaa: Rais Uhuru na DP Ruto walitumiana jumbe za makasiriko

Fri, 17 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Ijumaa Septemba 17 yameangazia taarifa kadhaa za matukio ya humu nchini kama vile uhasama wa kisiasa ambao unaendelea kati ya Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto.

Inaibuka kuwa tofauti zilizoko kati ya Rais na DP ni kali na huenda juhudi za viongozi wa kanisa kuwapatanisha zikagonga mwamba.

The Star

Kulingana na jarida hili, Rais Uhuru na Ruto walitumiana jumbe kali wakati ambapo urafiki wao kisiasa ulianza kufifia.

Haijabainika yaliyokuwa kwenye jumbe hizo lakini sasa viongozi wa kanisa wanasema tofauti kati ya wawili hao si tu za kisiasa mbali kibinafsi.

Wandani wanasema juhudi za kuwapatanisha wawili hao hapo awali zilifeli kutokana na uzito wa tofauti zao.

Viongozi wa kanisa hata hivyo wamerejelea juhudi tena huku DP akisema yuko tayari kwa maridhiano hayo.

People Daily

Taarifa kuu hapa ni kilio cha Wakenya kuhusu kuongezeka kwa gharama ya maisha na sasa wameitaka serikali kushukisha bei ya mafuta mara moja.



Wakenya wametishia kuzua maandamano ya kiuchumi iwapo bei hiyo haitashuka wakisema mzigo wa maisha umekuwa mzito zaidi.

Vigogo wa kisiasa pia wamezungumzia hilo huku Raila Odinga akisema ni jambo la kukera kuwa Wakenya bado wanakabiliwa na athari za Covid-19 lakini serikali inaongeza bei za mafuta.

"Wakenya ambao wamekuwa wakipambana na janga la Covid-19 sasa wameongezewa mzigo wa bei za juu za mafuta. Ni lazima bei hiyo ishukishwe," Raila alisema.

Daily Nation

Gazeti la Nation limeangazia handisheki kati ya Rais Uhuru na naibu wake William Ruto ambayo inapendekezwa na viongozi wa kanisa.

Nation imenukuu Ruto wakati wa kikao chake Karen Alhamisi aliposema yuko tayari kabisa kwa salamu na Rais.

Taifa Leo

Mhariri wa taifa leo anaangazia bei za mafuta ambazo zilipanda kwa zaidi ya KSh7 kwa kila lita ya diseli, petroli au mafuta taa.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke