Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Ijumaa: Rais Uhuru Akosa Kuwateua Majaji Waliosimamisha Reggae ya BBI

D2539ea6a85ddc51 Magazeti Ijumaa: Rais Uhuru Akosa Kuwateua Majaji Waliosimamisha Reggae ya BBI

Fri, 4 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais Uhuru Kenyatta Alhamisi Juni 3 aliwateua majaji saba watakaohudumu katika Mahakama ya Rufaa.

Rais aliteua saba hao wakiwa ni kati ya 34 ambao aliwaidhinisha kuhudumu katika mahakama ambazo Tume ya Idara za Mahakama JSC ilikuwa imependekeza.

1. People Daily

Jarida la People Daily limeangazia hatua ya Rais Kenyatta kuwaacha nje majaji wanne waliokuwa wamependekezwa na JSC kuhudu katika Mahakama ya Rufaa.

JSC ilikuwa imependekeza kuteuliwa kwa majaji 11 ili kuongeza idadi ya mahakama hiyo kutoka 19 hadi 30.

Walioteuliwa ni Msagha Mbogholi, Hellen Omondi, Mumbi Ngugi, Francis Tuiyot, Pauline Nyaboke, Jessie Lessit, na Kibaya Laibuta.

Rais aliwaacha majaji Joel Mwaura Ngugi, Weldon Korir, Aggre Muchelule na George Odunga.

Ngugi na Odunga ni baadhi ya majaji watano ambao walisimamisha reggae ya BBI baada ya kusema mswada huo haukufuata katiba.

2 The Star

Gazeti hili lina taarifa kuhusu aliyekuwa mwalimu mkuu wa shule ya wasichana ya Icaciri Jane Muthoni Juni 3 alifungwa mika a30 gerezani baada ya kupatikana na kosa la kumuua mumewe.

Muthoni na mshukiwa mwenza watahudumu kifungu hicho kwa kosa la mauaji ya aliyekuwa mwalimu mkuu wa shule ya Wavulana ya Kiiru.

Jaji Joel Ngugi alisema Muthoni ni mke hatari aliyepanga na kufadhili mauaji ya mumewe baada ya kushuku anaonja asali nje ya ndoa.

Gazeti hili pia lina taarifa kuhusu mzazi mmoja mtaani Kitengela ambaye anaomba haki baada ya mwanawe kuuawa kinyama.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke