Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Alhamisi, Juni 10: Waziri Yatani kusoma bajeti ya KSh 3.6 trilioni leo

2b3ff9788e2cc77b Magazeti Alhamisi, Juni 10: Waziri Yatani kusoma bajeti ya KSh 3.6 trilioni leo

Thu, 10 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Alhamisi, Juni 10, yameripotia kuhusu bajeti ya KSh 3.6 trilioni ya mwaka wa kifedha 2021/2022 ambayo inatazamiwa kusomwa na Waziri wa Fedha Ukur Yatani.

Magazeti haya pia yamegusia presha ambayo Rais Uhuru Kenyatta amelimbikiziwa na sehemu ya Wakenya na wataalam wa sheria baada ya kukataa kuwaapisha majaji sita wiki jana.

1. Daily Nation Gazeti hili linaripoti kuhusu kibarua kigumu kinacho msubiri Yatani huku akijaribu kuweka matumaini nchini kufuatia athari za janga la COVID-19.

Yatani anatazamiwa kusoma bajeti ya KSh3.6 trilioni leo Alhamisi, Juni 10, ya mwaka wa kifedha wa 2021-22.

Kulingana na gazeti hili, masuala ambayo yanamuumiza Yatani kichwa ni ikiwemo pesa za kufadhili miradi ya Rais Uhuru ya Ajenda Kuu Nne ya maendeleo.

Waziri huyo pia anakumbana na changamoto ya kukopa KSh930 bilioni kufadhili bajeti hiyo na kutimiza ahadi iliyotolewa kwa Shirika la Fedha Duniani (IMF).

2. Taifa Leo Gazeti hili linaripoti kuhusu hatua ya jaji mkuu wa zamani David Maraga kumkashifu Uhuru baada ya kukataa kuwaapisha majaji sita.

Maraga alisema kuwa utawala wa Uhuru utaharibika kwa kukiuka katiba.

Kwa upande mwingine, mtangulizi wa Maraga, Willy Mutunga, alielezea hatua ya rais kukataa kuwaapisha majaji sita kama matumizi mbaya ya mamlaka.

Mutunga, Jumanne, Juni 8, alimshutumu vikali Uhuru kwa kutumia vibaya mamlaka yake akisema ni hujuma.

3. The StandardThe Standard linaripotia kuhusu mpango wa wabunge kushinikiza Hazina ya Kitaifa kuongeza pesa za kulipa madeni ya muda mrefu ya wasamabzaji hatua ambayo itachangia deni la kitaifa kurundikana.

Pendekezo hilo ni la ripoti ya Kamati ya Bunge Kuhusu Bajeti kwenye mpango wa taifa kutumia pesa wakati wa mwaka wa kifedha wa 2021/2022 ambalo litawasilishwa bungeni leo asubuhi.

Ukaguzi uliofanywa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa niaba ya Hazina ya Kitaifa mwaka 2018 ulibaini kuwa serikali kuu na za kaunti zina madeni ya wasambazaji KSh 225 bilioni kuanzia miaka ya nyuma.

Kwa mfano Idara ya miundombinu inadaiwa kushikilia deni la KSh 85 bilioni na miradi 88 kusitishwa.

4. The Star The Star limeguzia sababu za Gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya na mwenzake wa Mombasa Hassan Joho kupiga abautani na kuanza kumuunga mkono kiongozi wa Orange Democratic (ODM) Raila Odinga kuwania urais 2022.

Kulingana na gazeti hili Oparanya na Joho walikuwa wamewasilisha maombi yao kuwania urais kupitia tikiti ya chama cha ODM katika chaguzi za 2022.

Siku moja iliyopita, Joho aliambia gazeti moja la humu nchin kuwa hataki kuwa miongoni mwa wanaomzuia Raila kumrithi Uhuru mwaka 2022.

Wachanganuzi wa siasa na wanasiasa ambao walizungumza na gazeti hilo walisema kuwa huenda Oparanya na Joho walifanya maamuzi ambayo yatamupa Raila nafasi kuwania kiti hicho kwa mara ya tano.

5. People Daily Gazeti hili limefichua wahusika wakuu katika taarifa za kila siku kuhusu hali ya COVID-19 nchini ambayo hutangazwa kila siku na Waziri wa Afya Mutahi Kagwe.

Watu hao hutumia muda wao siku mzima kupitia stakabadhi za COVID-19 na kushauri taifa kuhusu njia bora ya kuzuia ugonjwna huo.

Kikosi hicho kinaongozwa na Loice Achieng’ Ombajo ambaye ni mtaalamu wa magonjwa ya kuambukizana na Thumbi Mwangi ambaye ni mtaalam wa magonjwa.

Wawili hao hulala usiku wa manane baada ya kutoa data za COVID-19 na kushauri serikali hatua za kuchukua.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke