Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti, Alhamisi, Aprili 8: Wengi kufutwa kazi serikalini Kenya kupewa mkopo

6cb0cdc2a3939490 Magazeti, Alhamisi, Aprili 8: Wengi kufutwa kazi serikalini Kenya kupewa mkopo

Thu, 8 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Alhamisi, Aprili, 8, yameripotia kuhusu siasa za urithi 2022 ambapo wanawake wenye ushawishi watakuwa kwenye mstari wa mbele.

Magazeti haya pia yamegusia kwamba wandani wa Raila Odinga wamo kwenye njia panda kuhusu Mpango wa Maridhiano (BBI) uchaguzi mkuu unapokaribia.

1. Daily Nation Gazeti hili limeorodhesha majina ya wanawake wanane wenye ushawishi ambao wanatazamiwa kunogesha siasa za urithi 2022.

Nane hao ni:

Gavana wa Kitui Charity Ngilu - Waziri huyo wa zamani ni msemaji mkuu katika kubuni mirengo ya kisiasa

Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru- Gavana huyo anapigia debe BBI.

Aliyekuwa mama wa taifa Mama Ngina Kenyatta - Ni mshauri wa Rais Uhuru Kenyatta

Rachel Ruto - Mkewe Naibu Rais William Ruto anafahamika sana kwa siasa za mashinani.

Ida Odinga - Mke wa Raila Odinga ana ushawishi mkubwa kisiasa

Martha Karua - Kiongozi wa Narc Kenya anapinga BBI.

Nancy Gitau - Mshauri huyo wa zamani wa rais amekuwa akibuni mikakati ya siasa za Rais Uhuru Kenyatta

Margaret Kenyatta- Mama wa tiafa amaegusa nyoyo za wengi na kampeni zake

2. The Standard Watu wengi wanatazamiwa kupoteza kazi zao katika sekta ya umma kufuatia masharti makali yaliyotolewa na Shirika la Fedha Duniani (IMF) kabla ya kutoa mkopo wa KSh 255 bilioni.

Moja ya sheria za shirika hilo ni kudhibiti mashirika yanayomilikiwa na serikali kuanza kupata faida.

Hii ina maana kuwa wafanyakazi kadhaa wa serikali watafutwa kazi kama njia ya kutekeleza sheria hiyo.

Mkopo huo wa miaka mitatu unatazamiwa kusaidia katika vita dhidi ya COVID-19.

3. People Daily Mpango wa mwaka 2022 wa kiongozi wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM) Raila Odinga umewagawanya wandani wake wakuu.

Huku Raila akishikilia imani katika mchakato wa BBI na handisheki kati yake na Uhuru, baadhi ya wandani wake wanamtaka achukuwe msimamo wake.

Hatua ya rais kuunga mkono muungano wa One Kenya Alliance uliobuniwa na kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka, Moses Wetang'ula wa Ford Kenya, kiongozi wa Kanu Gideon Moi na Musalia Mudavadi wa Amani National Congress pia imeyumbisha ODM.

Mbunge wa Suba Kusini John Mbadi ambaye pia ni mwenyekiti wa ODM ni miongoni mwa wale ambao wanamtaka Raila aendeleze uhusiano wake na Uhuru akidai kuwa ukariba wao utaongezea uzito mwaka 2022.

4. The StarKaunti ziko kwenye hatari ya kukumbana na uhaba wa fedha kufuatia Wizara ya Fedha kuchelewa kutoa pesa.

Mnamo Jumatano, Aprili 7, magavana walisema wizara hiyo bado haijatoa pesa kwa miezi mitatu huku janga la COVID-19 likikeketa.

Bado gatuzi hazijapata KSh 85.2 bilioni, ikisalia miezi miwili mwaka wa kifedha wa 2020/2021 kutamatika.

5. Taifa Leo Serikali imebabaishwa na kampeni za Wakenya mitandaoni baada ya kuchukua mkopo mwingine wa KSh 255 bilioni kutoka IMF.

Wakenya wamekita kambi kwenye mitandao ya kijamii wakitaka IMF kufuta mkopo huo.

Serikali imeanza msako unaowalenga wanaharakati walio kwenye mstari wa mbele kuendesha kampeni hizo mtego wa kwanza ukimpata mwanaharakati Edwin Kiama.

Kiama alikamatwa Jumanne, Aprili 6, kwa madai ya kuchapisha notisi tata dhidi ya Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke