Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mafuta yapanda bei Kenya

E71882e2 8676 4b7c 83b8 D2abfd5ed339 Mafuta yapanda bei Kenya

Thu, 15 Sep 2022 Chanzo: BBC

Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Petroli nchini Kenya imetangaza bei mpya za mafuta.

Katika mabadiliko hayo, lita moja ya mafuta ya petroli itauzwa kwa Sh179.30, bila ruzuku ikiwakilisha ongezeko la Sh20.18.

Kwa upande mwingine, bei ya dizeli imeongezeka kwa Sh25 na sasa itauzwa kwa Sh165 jijini Nairobi.

Bei ya Mafuta ya Taa imeongezeka kwa Sh20 kumaanisha kuwa itauzwa Sh147.94 jijini Nairobi.

Bei hizo ni pamoja na asilimia 8 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT).

Kupanda kwa bei ya mafuta kunafuatia kuondolewa kwa ruzuku ya mafuta kwa bidhaa za petroli na serikali ya Rais William Ruto .

Ingawa ruzuku ya petroli imeondolewa, ruzuku ya Sh20.82 kwa lita na Sh26.25 kwa lita ilihifadhiwa kwa dizeli na mafuta ya taa mtawalia.

Mabadiliko ya bei ya mafuta yanaanza kutekelezwa mara moja.

Ongezeko hilo linamaanisha kuwa gharama ya ya maisha inatarajiwa kupanda wakati bei za bidhaa za viwandani zinapoanza kuongezeka, kwa sababu ya ongezeko linalofuatia la gharama ya umeme.

Vile vile, gharama ya usafiri na umeme itapanda kwa sababu Kenya inaongeza malipo ya ya mafuta kwenye bili za umeme.

Ni gharama ya juu zaidi ya nishatinchini Kenya.

Serikali ya Kenya inasema imetumia takriban dola bilioni 1.2 katika mwaka uliopita kuweka bei ya mafuta chini kupitia ruzuku huku bei ya bidhaa hiyo ikipanda katika soko la kimataifa.

Kumekuwa na mseto wa maoni mitandaoni nchini humo kuhusu ongezeko hilo Serikali mpya ya rais Ruto imesema ruzuku imeondolewa kwa sababu haijawasaidia Wakenya.

Chanzo: BBC