Hapa ndipo Derna inapokutana na bahari.
Na ni pale ambapo, hata karibu wiki moja baada ya mafuriko haya kutokea, miili bado inasombwa.
Unaweza kuona uchafu wote - kuna magari yaliyoharibika, matairi, mbao zilizovunjika, vifaa vya nyumbani, jokofu, friza, kila aina ya vitu vikichanganywa pamoja vinavyoelea na kuingia maji ndani ya maji.
Kuna harufu nzitoya maji taka na kifo.
Nimekuwa nikizungumza na timu ya uokoaji ya Uturuki ambayo imekuwa hapa kwa siku 5 zilizopita.
Wanatembea wakitafuta miili inayoingia kwenye mawimbi na kunaswa kati ya uchafu huu wote.
Wanasema wameondoa miili mitatu leo asubuhi kutoka eneo hili.