Thu, 11 May 2023
Chanzo: Bbc
Miili zaidi inaendelea kupatikana karibu wiki moja baada ya maporomoko ya ardhi katika eneo la Kalehe mashariki mwaJamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Msemaji wa Serikali ya Congo Patrick Muyaya amethibitisha kwamba kufikia sasa watu 438 wamefariki, mamlaka zinasema huenda idadi hiyo ikaongezeka kwa sasabu kuna wale ambao bado hawajapatikana.
Mashirika ya kiraia yanakadiria kuwa watu 5,000 hawajulikani walipo.
Gavana Theo amesema manusura watahamishwa kwa muda katika uwanja wa ndege wa Luena.
Chanzo: Bbc