Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Madaktari feki wanaswa wakitoa chanjo bandia ya COVID-19

0fgjhs630nh4ifccd Madaktari feki wanaswa wakitoa chanjo bandia ya COVID-19

Wed, 15 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Wanaume wawili wamefikishwa kortini Jumanne, Septemba 15, kwa kutoa chanjo feki ya COVID-19 ya Johnson and Johnson.

Wawili hao wanakabiliwa na mashtaka kumi na moja ikiwemo kupokea KSh 200,000 kwa njia ya utapeli kutoka kwa watu waliodaiwa kudungwa chanjo hiyo.

Wawili hao walikuwa wakijifanya madaktari kutoka Hospitali Kuu ya Kitaifa ya Kenyatta(KNH) kwa kughushi vitambulisho vya hospitali hiyo.

Walikuwa wakitibu watu katika hospitali ya kibinafsi ya Crane Hospital kwa kipindi cha miaka minne.

Madaktari hao bandia, Wallace Mugendi Njiru na Kenneth Mukundi Njiru walikabiliwa na mashtaka kumi na moja ikiwemo kupokea KSh 200,000 kwa njia ya utapeli kutoka kwa watu waliodaiwa kudungwa chanjo hiyo kati ya Agosti 10 na Agosti 13 2021.

Kwa mujibu wa Taifa Leo, wawili hao pia wanakabiliwa na mashtaka ya kujifanya madaktari kutoka Hospitali Kuu ya Kitaifa ya Kenyatta(KNH) huku wakighushi vitambulisho vya hospitali hiyo.

Pia walighushi leseni ya hospitali ya kibinafsi.

Wawili hao walifikishwa mbele ya Hakimu Mwandamizi wa Mahakama ya Milimani Martha Nanzushi ambapo mahakama ilifahamishwa kuwa walijifanya kuwa madaktari kati ya Julai, 24 2017 na Septemba 7, 2021.



Walikuwa wakiendeleza udanganyifu wa katika eneo la Roysambu, Kasarani kaunti ya Nairobi ambapo walikuwa wakitibu watu katika hospitali ya kibinafsi ya Crane Hospital.

Kesi hiyo itatajwa tena baada ya wiki mbili.

Wakili feki akamatawa kortiniKwingineko, wakili feki ambaye alijifanya mtaalam wa sheria mbele ya hakimu amenaswa.

Inaripotiwa kwamba Adeola Babatunde amekuwa akiwakilisha wateja wake kortini, kwa miaka 10 bila makaratasi halali.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Nigeria, wakili huyo alikuwa amefika mbele ya Hakimu A. A Adeyeba in Osogbo wa Jimbo la Osun State mnamo Machi 10, 2021, ambapo alikuwa anatakiwa kuwasilisha hoja wakati ujanja wake ulitambulika.

Wakili huyo alizua shauku kutokana na namna alikuwa akiwasilisha hoja yake na kumkasirisha mmoja wa mawakili kortini.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke