Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Madagascar: Watakaobaka watoto kuhasiwa

Ubakajiiii Madagascar: Watakaobaka watoto kuhasiwa

Fri, 9 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Bunge la Madagascar limeidhinisha sheria mpya ambayo itawafanya watu waliopatikana na hatia ya unyanyasaji wa kingono kwa watoto kuhasiwa na kuhukumiwa kifungo cha maisha jela.

Kwa mujibu wa sheria mpya, wanaopatikana na hatia ya kubaka watoto wenye umri kati ya miaka 10 hadi 13, watahasiwa kwa kemikali na kifungo cha miaka 15 hadi 20 pamoja na kazi ngumu, lakini ikiwa mkosaji ni mdogo, hatapata adhabu ya kuondolewa kiungo chake.

Hayo yamejiri siku chache baada ya Kazakhstan kuwasilisha sheria sawa na hiyo kutokana na wabunge wa eneo hilo kushutumu kuwa kuhasiwa kwa kemikali, adhabu iliyotolewa kwa wabakaji kwa watoto, kumeshindwa kukomesha watu kufanya uhalifu huo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live