Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Madagascar: Serikali yatibua njama ya kumuua Rais Andry Rajoelina

7ff7052e00ebbdaf Madagascar: Serikali yatibua njama ya kumuua Rais Andry Rajoelina

Fri, 23 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais Andry Rajoelina aliponea jaribio la mauaji baada ya mwanasheria mkuu kuzima njama ya washukiwaBerthine Razafiarivony alisema washukiwa walikamatwa siku ya Jumanne, Julai 20, baadhi wakiwa raia wa nchi za kigeniWashukiwa pia wanadaiwa kupanga njama ya kuwauwa viongozi na wanasiasa wakuuRajoelina aliaapishwa kuwa rais wa Madagascar mwaka wa 2019 baada ya uchaguzi uliokumbwa na ushindani mkali kutoka kwa mpinzani wakeRais wa Madagascar Andry Rajoelina ameponea jaribio la mauaji baada ya mwanasheria mkuu wa nchini hiyo kutibua njama ya washukiwa.

Akizungumza na vyombo vya habari, mwanasheria mkuu Berthine Razafiarivony alisema washukiwa walikamatwa na wanasemekana kuwa wa nchi za kigeni.

Washukiwa wanazuiliwa huku uchunguzi kuhusu kile mwanasheria huyo alikitaja kama'Shambulio dhidi ya Serikali'.

" Raia kadhaa wa nchi za kigeni na wengine wa Madagasca walikamatwa siku ya Jumanne, Julai 20 wakiwa ni washukiwa wakuu wa jaribio la mauaji kwa Rais," Taarifa kutoka kwa afisi ya mwanasheria mkuu ilieleza.



Read also

Isiolo: Afisa Aliyerusha Bomu Akimlenga "EX" Wake Akosa Shabaha na Kulipua Nyeti za Mwanajeshi

Razafiarivony aliongezea kwamba kando na kujaribu kumuua Rais, serikali pia ilitibua njama ya kuwauwa viongozi na wanasiasa wakuu.

Hata hivyo, haijabainika raia waliokamatwa walitokea nchi zipi lakini uchunguzi unaendelea dhidi yao.

Rajoelina aliaapishwa kuwa rais wa Madagascar mwaka wa 2019 baada ya uchaguzi uliokumbwa na ushindani mkali kutoka kwa mpinzani wake ambaye alipinga ushindi wa Rais huyo katika mahakama ya kikatiba.

Marc Ravalomanana ambaye alikuwa mpinzani wake mkuu na mtangulizi wake pia, alidai uchaguzi wa Disemba 2018 ulikumbwa na udanganyifu na wizi wa kura.

Kwingineko, Rais Assimi Goïta alinusurika kifo Jumanne, Julai 20, 2021 baada ya watu wawili kujaribu kumuua kwa kumdunga kisu akiwa kwenye msikiti mji mkuu Bamako.

Goita alikuwa amejumuika na waislamu wenzake kuhudhuria ibada ya siku kuu ya Eid ul-Adha katika msikiti wa Grand Mosque.

Washukiwa walikamatwa na Rais huyo kuondolewa msikitini akiwa salama.



Read also

Uchunguzi wa Maiti Waonyesha Christine Ambani Aliuawa kwa Kudungwa Kisu Shingoni

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke