Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mabloga wa DP Ruto mahakamani, barua kuhusu njama ya kummaliza DP yawaandama

446a9f4f6d04f2d0 Mabloga wa DP Ruto mahakamani, barua kuhusu njama ya kummaliza DP yawaandama

Wed, 16 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mkachero wanasema uchunguzi wao ulionyesha barua hiyo ilitoka kwa simu ya Gateri kabla ya Itumbi kuisambazaKachero Ruto alisema barua hiyo iliwasha joto la kisiasa hadi Itumbi akaamua kuifuta kutoka mitandaoniIlikuwa imedai viongozi wa mloima Kenya walikuwa wamefanya mkutano katika mkahawa wa La Mada kupanga kuhusu mauaji ya DP RutoKesi inayowahusu wanablogu Dennis Itumbi na Samuel Gateri kuhusu barua iliyodai kulikuwa na njama ya kumuua Naibu Rais William Ruto imeanza kuskizwa.

Itumbi na Gateri walifika mahakamani Jumanne Juni 15 kuhusu barua hiyo huku upande wa mashtaka ukisema ndio walikuwa waandishi wa barua hiyo.

Ilidai kikao kilikuwa kimefanywa na viongozi kadhaa wakiwamo mawaziri ambao walipanga kummaliza DP Ruto kwa ajili ya siasa za 2022.

Kulingana na afisa aliyechunguza suala hilo Isaac Ruto, barua hiyo ilichapishwa kutoka simu ya Gateri kabla ya Itumbi kuisambaza kwenye mtandao wa WhatsApp.



Mbele ya hakimu mkuu wa Milimani Martha Mutuku, Ruto alisema wawili hao walikuwa na nia ya kuzua wasiwasi nchini.

Alsiema Itumbi baadaye aliamua kufuta barua hiyo baada ya kugundua kuwa ilikuwa imezua wasiwasi mkubwa nchini.

Barua hiyo ilisema kikao cha kupanga mauaji hayo kilifanyika katika hoteli ya La Mada katika barabara ya Thika.

Mawaziri James Macharia wa Uchukuzi, Joseph Mucheru wa Teknolojia, Sicily Kariuki wa AFya na Peter Munya wa Biashara walidaiwa kuhudhuria kkikao hicho.

Mawaziri hao walidhibitisha kuwa na kikao kwenye mkahawa huo lakini Munya kwa niaba ya wenzake wakapuuza kujadili njama hiyo.

Ni barua iliyozua joto la kisiasa humu nchini kiwango cha DP Ruto kujadili suala hilo huku wandani wake wakitaka apewe ulinzi zaidi.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke