Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Maandazi 7 na sigara 9 zamfunga jela miaka 15

4f61688203ab416c Maandazi 7 na sigara 9 zamfunga jela miaka 15

Wed, 18 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mnamo 2013, Andrew Arinaitwe Kasasira alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani kwa wizi. Aliamua kukata rufaa akidai kuwa uamuzi wa kwanza haukuwan sawa kwa kile alikitaja alifanya makosa madogo tuHata hivyo, matumaini yake yalivunjwa wakati jopo la majaji watatu lilishikilia uamuzi wa awaliAndrew Arinaitwe almaarufu Kasasira atatumikia kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kuiba mandazi saba na vijiti tisa vya sigara.

Hii ni baada ya mahakama ya Uganda kushikilia uamuzi wa awali ukitaja kisa hicho kama wizi.

Aiba pesa, mandazi na sigaraKwa mujibu wa Daily Monitor, kesi hiyo ilisikizwa mara ya kwanza mjini Masaka na uamuzi ulitolewa na Jaji Margaret Oumo-Oguli mnamo Aprili 25, 2013.

Mahakama ilifahamishwa kuwa mnamo Mei 21, 2012, Kasasira aliingia katika duka linalomilikiwa na Bi. Nazziwa akinyonyesha na kuchukuwa sigara, mandazi, na USh 15,000 (KSh 460) pesa taslimu.

Nazziwa alishuhudia kuwa alitoka nje kuchunguza kilichokuwa kikiendelea baada ya kusikia sanduku lake la pesa likifunguliwa dukani.

"Wakati Kasasira alimuona Nazziwa, alichomoa kisu ndani ya suruali yake na kumuonyesha. Hata hivyo, mwathiriwa alikuwa jasiri na kumpokonya Kasasira kisu hicho," ilisoma ushuhuda wa Nazziwa.

Mtafaruku huo uliwavutia wapita njia ambao walimbia kumuokoa Nazziwa na kupambana na mshtakiwa.

Kisu ambacho alijaribu kumtishia mama huyo, kilipatikana pamoja na mandazi saba, vijiti tisa vya sigara na pesa.

Akata rufaaLicha ya kukiri makosa yake, Kasasira hakuridhishwa na uamuzi huo na kuamua kuwasilisha kesi ya rufaa katika Mahakama ya Rufaa akitaka kesi hiyo kusikizwa upya.

Kulingana naye, jaji alifanya makosa kwa kumhukumu miaka 15 gerezani, ambapo si sawa kwani makosa yake yalikuwa madogo.

Rufaa hiyo ilisikwa na jopo oa majji watatu wab Majakama ya Rufaa, Stephen Musota, Cheborion Barishaki, na Muzamiru Mutangula Kibeedi.

Baada ya kusikiza rufaa hiyo kwa makini, majaji hao waliamua kwa kauli moja kuwa mshtakiwa anastahili adhabu hiyo aliyopewa awali.

"Hukumu ya Mahakama Kuu ya miaka 15 gerezani kwa kupatikana na hatia ya wizi kinyume cha kipengele cha 285 na 286(2) cha sheria inashikiliwa," ilisoma uamuzi huo.



Hukumu ya Kasasira ilisomwa bila yeye kuwepo kutokana na masharti ya COVID-19 huku akiwakilishwa na wakili wake Lawrence Yawe.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke