Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Maandamano yazuka kukashifu kuondolewa kwa maafisa wa usalama wa Ruto

08f5b440bf8c62df Maandamano yazuka kukashifu kuondolewa kwa maafisa wa usalama wa Ruto

Thu, 26 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Kundi la vijana lilifika Sugoi na kusema liko tayari kutoa ulinzi kwa DP baada ya ripoti kuwa maafisa wa GSU wameondolewaBaadaye maandamano yalizuka mjini Eldoret kukashifu hatua ya GSU hao kuondolewa huku wafuasi wa DP wakisema ni hujuma kubwaWaziri wa Usalama Fred Matiang'i alidaiwa kucheza siasa katika kuchukua hatua hiyo iliyozua joto la kisiasaKundi la vijana kutoka Uasin Gishu limefika nyumbani kwa naibu rais William Ruto huko Sugoi wakisema wako tayari kumpa ulinzi baada ya maafisa wake wa GSU kuondolewa.

Vijana hao walisema wamekerwa na hatua ya serikali kuondoa maafisa wa GSU nyumbani kwa DP lakini wako tayari kushika doria humo.

Aidha maandamano pi yalizuka mjini Eldoret huku wakazi wakisema ni lazima DP arudishiwe walinzi wake.

Walilaumu waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i wakisema anatumiwa kumhujumu DP kisiasa.

"Matiang'i ni lazima aende. Hii ni madharau," waandamanaji hao walisema.

"Hatuwezi kukubali kuwa mkuu wa polisi aondoe usalama wa DP. Tunataka kujua ni nia gani mko nayo katika kutoa usalama wa DP," mwakilishi wa kina mama Gladys Shollei alisema.





Mbunge wa Bahati Kimani Ngunjiri alisema kuondolewa kwa usalama wa DP ni njama ya maadui wake.

"Ile maneno Atwoli alisema sasa inaonekana inaendelea kufanywa. Alisema naibu rais hatakuwa kwenye uchaguzi ujao. Inaonekana sasa hilo ndilo linapangwa," alisema Ngunjiri

Hatua ya kuwaondoa maafisa hao wa usalama ilizua hisia kali huku Mbunge Oscar Sudi akilaumu Rais Uhuru Kenyatta.



"Rais na Matiang'i wameagiza maafisa wa usalama waliokuwa wakilinda Sugoi, Elgon View, Karen na mali zingine zinazohusishwa na DP Ruto. Ujinga mtupu!" alisema Sudi.

Kulingana na msemaji wa Ruto, David Mugonyi, mabadiliko hayo ya maafisa wa usalama yamefanywa pasi maelezo yoyote.

Msemaji wa kikosi cha polisi Bruno Shioso alisema maafisa wa AP waliopelekwa kwa DP ni kutoka kitengo spesheli cha kulinda majengo ya serikali.

Alisema kikosi cha usalama wa rais ndicho kitaendelea kumlinda DP akitaja mageuzi hayo kama suala la kawaida.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke