Mwanafunzi aliyetambulika kwa jina la Joel Shindani Malu (27) raia wa Congo DR, amefariki dunia akiwa mikononi mwa Jeshi la Polisi katika mji wa Bengaluru nchini India.
Polisi nchini humo wanadai kuwa kijana huyo alipatikana akifanya biashara ya dawa za kulevya huku pia akiwa na vidonge vya maradhi ya saikolojia. Hata hivyo maelezo ya Jeshi hilo yammeonekana kama ngonjera kwa waandamanaji wakikundi cha kutetetea haki za wanafunzi wa kiafrika nchini humo kinachoitwa "Pan African Federation" hali iliyopelekea waandamanaji sita wa kiafrika kujeruhiwa vibaya
Hadi sasa Jeshi la Polisi nchini humo bado linafanya uchunguzi wa kina kubaini chanzo kifo cha mwanafunzi huyo.