Wed, 26 Jun 2024
Chanzo: Bbc
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameelezea wasiwasi wake kuhusu matukio yaliyoshuhudiwa katika maandamano ya kupinga muswada wa fedha nchini Kenya.
''Nimesikitishwa sana na ripoti za vifo na majeruhi - ikiwa ni pamoja na waandishi wa habari na wafanyikazi wa matibabu - yaliyohusishwa na maandamano ya mitaani nchini Kenya.''
Bw. Guterres ametoa wito kwa mamlaka za Kenya zijizuie, na kuwaomba wanaoshiriki maandamano kufanya hivyo kwa amani.
Chanzo: Bbc
Related Articles: