Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki wanatarajiwa kuhudhuria Mkutano wa 18 wa Kilele wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaofanyika Jumatano, Desemba 22, 2021.
Mkutano huo utakaofanyika kwa njia ya mtandao, unatarajiwa kujadili na kuamua kuhusu kuingizwa kwa DRC katika jumuiya ya EAC.
Mkutano huo utatanguliwa na Mkutano wa Ziada wa 45 wa Baraza la Mawaziri wa EAC, unaokaofanyika leo Jumatatu, Desemba 20, 2021.
Mkutano huo unatarajiwa kuzingatia mambo mawili; ripoti ya Baraza la Mawaziri kuhusu kukubaliwa kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika EAC na marekebisho ya Kanuni ya Akidi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi za EAC.
Mkutano wa Ziada wa Kawaida utaonyeshwa moja kwa moja kwenye tovuti ya EAC - www.eac.int pamoja na majukwaa mengine ya mitandao ya kijamii ya EAC.