Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Maambukizi ya COVID-19 yapanda, watu 486 waugua huku 18 wakifariki

26cc99c3f6ed8de0 Maambukizi ya COVID-19 yapanda, watu 486 waugua huku 18 wakifariki

Mon, 12 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Idadi jumla ya maambukizi ya COVID-19 nchini imeongezeka hadi 145,670 baada ya watu wengine 486 kunasa virusi hivyo

- Katika visa hivyo vipya, 463 ni Wakenya na 23 ni raia wa kigeni ambapo 278 ni wnaume na wanawake 208

- Wagonjwa wengine 490 wamepona ugonjwa huo ambapo 172 walikuwa wanapokea matibabu na wenginege 318 walikuwa wamelazwa katika hospitali nchini

Watu 486 wamepatikana na virusi vya corona kutoka kwa sampuli 4,134 zilizopmwa chini ya saa 24 huku idadi jumla ya maambukizi nchini ikiongezeka hadi 145,670.

Kulingana na taarifa ya Wizar ya Afya, kutoka kwa visa hivyo vipya, 463 ni Wakenya na 23 ni raia wa kigeni ambapo 278 ni wanaume na wanawake 208.

Mgonjwa mwenye umri mdogo ni mtoto wa miezi mitatu na mzee zaidi ana miaka 94.

Wakati huo huo vifo 18 vimeripotiwa kutokana na virusi hivyo ambapo waathiriwa waliangamia tarehe tofauti huku idadi ya vifo ikiongezeka hadi 2,348.

Habari njema ni kwamba wagonjwa 490 wamepona ugonjwa huo ambapo 172 walikuwa wanapokea matibabu na wenginege 318 walikuwa wamelazwa katika hospitali mbali mbali.

Kwa sasa jumla ya watu 1,660 wamelazwa katika hispitali mbali mbali nchini huku wagonjwa 5,994 wakipokea huduma za matibabu nyumbani.

Wagonjwa 256 wamelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU), 44 wamewekwa kwenye mashine ya kuwasidia kupumua na wengine 181 wanaongezewa oksijeni. Wagonjwa 31 wanachunguzwa.

Wengine 257 wamewekwa kwenye oksojeni, 236 wamelazwa katika vymba vya kawaidia na wagonjwa wengine 21 katika chumba cha wagonjwa mahututi zaidi (HDU).

Msambao katika kauntiVisa vya maambukizi katika kaunti ni kama ifuatavyo:

Nairobi 264, Kiambu 35, Kitui 20, Nakuru 19, Nyamira 17 Kajiado 14, Kilifi 14, Machakos 13, Mandera 12, Mombasa 11 Nandi 10, Uasin Gishu 10, Meru 9, Kisumu 9, Nyeri 8, Homa Bay 5, Turkana 5, Kericho 3, Kisii 2, Laikipia 2, Lamu 1, Migori 1, Murang’a 1 na Tharaka Nithi 1.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke