Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Maafisa wa DCI watibua njama ya wizi, wawapiga risasi majambazi 2

Afbb1eac32e41d09 Maafisa wa DCI watibua njama ya wizi, wawapiga risasi majambazi 2

Fri, 23 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Makachero kutoka Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) walitibua jaribio la uhalifu liliokiwa limepangwa kutekelezwa na genge la majangili katika duka la vyuma mtaani Eastleigh Jumatano, Julai 21.

Taarifa ya DCI ilionyesha kuwa sita hao walikuwa wamevunja duka la kuuza vyuma la Jamarat eneo la Eastleigh 4th Street kabla ya kufumaniwa na maafisa kutoka Kituo cha polisi cha Pangani.

Maafisa hao waliokuwa wamepokea bahari kutoka kwa wananchi walifanikiwa kuwapiga risasi na kuwaua majangili wawili waliokuwa wakijaribu kuhepa.

Wanne kati yao hata hivyo walifanikiwa kutoroka.

"Awali majangili hao waliwasili katika duka hilo wakiwa kwenye gari la aina ya pickup kutekeleza uhalifu huo lakini maafisa wa polisi walifika kwa wakati ufaao na kuwatimua.

"Walikuwa wamejihami kwa bastola na walipofumaniwa walianza kuwafyatulia risasi maafisa lakini polisi hao waliyakwepa," taarifa ya DCI ilsiema.

Maafisa hao walifanikiwa kupata bastola, risasi tatu na silaha zingine hatari.

Vile vile matanki mawili ya maji ambayo washukiwa walikuwa wamepanga kuiba yalipatikana.



Read also

Askari Jela Akamatwa kufuatia Tuhuma za Visa vya Utekaji Nyara

Maafisa hao kwa sasa wamo mbioni kuwasaka washukiwa wanne waliohepa

Kisa hicho kinajiri siku moja baada ya mshukiwa wa ujambazi kukamatwa na maafisa wa polisi waliokuwa wakipiga doria mtaani Kasarani Jumanne, Julai 20, 2021 majira ya asubuhi.

Polisi pia waliweza kunasa bunduki kutoka kwa mshukiwa huyo.

Kulingana na maafisa wa upelelezi kutoka Idara ya DCI, mshukiwa ambaye hawakumtaja jina alikuwa amejaribu kutoroka kwa piki piki bila mafanikio.

Polisi walisema kwamba mshukiwa alianguka kutoka kwa piki piki baada ya polisi kumfuata wakiwa kwenye gari lao la Land Cruiser.

Akiwa na matumaini bado ya kutoroka, mshukiwa anasemekana kukabiliana na polisi kwa kuwafyatulia risasi lakini alipigwa na kujeruhiwa.

"Bila ya kushindwa, mshukiwa alikabili polisi kwa kufyatulia risasi gari lao, polisi mmoja alimpiga risasi na kumjeruhi vibaya ndiposa akakamatwa," Ripoti ya DCI.

Polisi wanaamini kwamba mshukiwa ni mmoja wa genge kubwa linalowahangaisha wakazi wa mitaa za Githurai na Kasarani.



Read also

Caroline Kangogo: Familia ya Afisa Aliyejiua Yasema Mwanao Atazikwa Kwao Jumamosi

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke