Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Maafisa 5 wa Jeshi wanaswa wakijivinjari kilabuni usiku

1167c60e41d836d6 Maafisa 5 wa Jeshi wanaswa wakijivinjari kilabuni usiku

Sat, 10 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Takriban maafisa watano wa Kikosi cha Jeshi (KDF) ni miongoni mwa watu 52 waliokamatwa na polisi huko Kisumu baada ya kupatikana wakinywa pombe majira ya usiku.

Watu hao walikamatwa asubuhi ya Jumamosi, Aprili 10, katika kilabu maarufu huko Lolwe Estate.

Polisi walilazimika kufyatua vitoa machozi ili kuwatimua walevi hao amabo walikuwa wamejifungia ndani ya baa hilo.

Kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Kisumu ya Kati Joseph Ng’etich ambaye aliongoza operesheni hiyo alisema waliokamatwa walipelekwa katika Kituo Kikuu cha Polisi cha Kisumu.

Watu hao watafikishwa mahakamani Jumatatu, Aprili 12.

Polisi walisema watashtakiwa kwa kukiuka amri za kutotoka nje, kukosa kuvaa maski na vile vile kurundikana katika eneo hilo la burudani.

"Jana saa 11.30 jioni, kikosi cha upelelezi kikiongozwa na kamanda wa polisi Kisumu Central kilifanya operesheni katika eneo la Lolwe Estate ambapo watu 52 walikamatwa kwa kukiuka itifaki za Covid-19," alisema Ng'etich.

Rais Uhuru Kenyatta alitangaza amri ya kutotoka nje majira ya usiku na hata kufunga kaunti za Nairobi, Nakuru, Kiambu, Machakos na Kajiado wakati taifa linakabiliana na wimbi la tatu la COVID-19.

Wakati uo huo, zaidi ya watu 40 walikamatwa Ijumaa usiku wakinywa pombe katika baa majira ya usiku eneo la Meru ambalo liko mpakani mwa Meru-Laikipia.

Walevi hao walikuwa wamejifungia ndani ya baa wakijifurahisha.

Walipofumaniwa, baadhi walijificha chini ya viti na wengine nao 10 wakahepa kupitia darini.

Hatimaye, zaidi ya watu 31 walikamatwa katika operesheni hiyo ambayo iliendelea hadi saa tisa asubuhi.

Miongoni mwa waliokamatwa walikuwa maafisa wa kaunti ya Nyandarua waliokuwa wakielekea kaunti ya Meru kwa sherehe ya mahari Jumamosi.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke