Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

MAGAZETI KENYA: Wakenya walidungwa maji na kutapeliwa ni chanjo ya Covid-19

940b656947bad52c MAGAZETI KENYA: Wakenya walidungwa maji na kutapeliwa ni chanjo ya Covid-19

Thu, 9 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Siasa za Mlima Kenya zimeangaziwa kwenye magazeti ya Alhamisi Septemba 9 haswa baada ya Gavana wa Kirinyaga Ann Waiguru kuashiria kuwa anapania kuhepa mrengo wa Rais Uhuru Kenyatta.

Aidha kuna taarifa pia kuhusiana na mapigano yanayoshuhudiwa katika kaunti ya Laikipia duru zikiarifu wanajesh watatumwa eneo hilo kukabiliana na bandits.

1. Star

Gazeti la Star limeipa taarifa za Gavana Ann Waiguru kuashiria huenda akahama kutoka chama cha Jubilee kuelekea uchaguzi mkuu ujao.

Waiguru anasema ni wazi kuwa itakuwa vigumu kushinda uchaguzi ujao na chama cha Jubilee kinachoongozwa na Rais Uhuru Kenyatta.

Mwandishi wa gazeti hilo anasema hatua ya Waiguru ni ishara ya wazi jinsi siasa za Mt Kenya zimebadilika na sasa hawatambui Jubilee ya Rais Uhuru.

Aidha kuna ripoti pia za kifo cha mwanaharakati Orio Rogo Manduli ambaye alifariki dunia hapo jana.

Orio alikuwa ni mama aliyeteka wengi kutokana na mtindo wake wa wmavazi na pia ukakamavu katika kuelezea masuala sugu kwenye jamii.



2. People Daily

Gazeti la People Daily lina taarifa kuhusu watapeli ambao waliwadunga Wakenya maji huku wakiwalaghai kuwa ni chanjo ya Covid-19.

Inaarifiwa jamaa wawili tayari wameshtakiwa kwa kuwapa Wakenya chanjo ya maji waksiema ni Covid-19.

Kundi hilo la wakora lilikuwa likiwalipisha wateja wao 3500 kwa kupata chanjo hiyo feki.

Nation

Gazeti hili limeangazia masaibu ndani ya kambi ya kisiasa ya DP Ruto ambapo inaarifiwa kumezuka mgogoro kuhusu miungano.

Kwa mujibu wa duru za kuaminika, Ruto anataka wandani wake wawe ndani ya chama kimoja cha UDA ilhali baadhi yao wamepinga hilo.

Mbunge Moses Kuria na aliyekuwa waziri Mwangi Kiunjuri wamesisitiza ni lazima wawe na vyama vyao na kisha kufanya muungano na UDA.

Standard

Jaji Said Chitembwe amekiri kuwa makachero wa DCI walipata fedha latika afisi yake walipomvamia Julai 22.

Alisema fedha hizo dola 7000 zilikuwa karo ya mwanawe aliye Australia na alikuwa akisubiri kuzipelekea benki.

Taifa Leo



Taariffa hapa ni kuhusiana na kukamatwa kwa wanasiasa wawili wanaohusishwa na mashambulzii yanayoendelea Laikipia.

Mbunge William Kamket na aliyekuwa mbunge wa Laikipia Kaskazini Mathew Lempurkel walikamatwa na kuhojiwa kuhusu mashambulzii hayo.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke