Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

MAGAZETI KENYA: Rais Uhuru abanwa azungumzie mabilioni aliyoficha majuu

18a49d829349314e Rais Uhuru abanwa azungumzie mabilioni aliyoficha majuu

Wed, 6 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatano yanripoti kuwa kinara wa ODM Raila Odinga ana nafasi kubwa sana ya kuingia Ikulu 2022 baada ya kuonekana kuungwa mkono na Rais Uhuru Kenyatta.

Kuna taarifa kuwa chama cha ODM kinapendekeza kuongezwa kwa idadi ya mawaziri wakisema hali ya sasa inamnyima rais nafasi ya kugawa mamlaka kwa kila eneo humu nchini.

1. Star

Gazeti hili lina taarifa kuhusu mbinu ambapo naibu rais William Ruto anajaribu kutumia kupambana na kinara wa ODM Raila Odinga kisiasa.

Ruto amekuwa akirudi eneo ambalo Raila amezuru katika kuajribu kuharibu kadi ambazo Raila hupanga akitangulia.

Hilo limeshuhudiwa katika eneo la Magharibi, Mt Kenya na Narok ambapo Ruto alizuru mara tu baada ya vikao vya Raila.

Aidha jarida hili limeangazia pia bahati ya Raila kuungwa mkono na Rais Uhuru Kenyatta kwani sasa wazito wengine serikalini na pia wa kibiashara wamekubali kumpa kura zao na usaidizi wa kifedha pia kuelekea 2022.

2. Standard

Gazeti hili limeangazia kifo cha wakili mashuhuri Evans Monari ambaye alifariki Jumanne asubuhi kwa mujibu wa ripoti za familia.

Monari alikuwa sugu wa kesi na alikuwa miongoni mwa kikosi cha mawakili kilichokuwa kikimtetea Rais Uhuru Kenyatta katika mahakama ya ICC huko Hagua baada ya kuhusishwa na kesi za ghasia 2007/08.

Mhariri wa jarida hili pia amepekua kiongozi wa ANC Musalia Mudavadi na azma yake ya kuingia Ikulu.

Mwandishi anasema licha ya kuwa Rais Kenyatta anaonekana kumuunga mkono kinara wa ODM Raila Odinga, huenda Mudavadi ndiye kadi fiche itakayorushwa 2022.

3. Nation

Rais Uhuru Kenyatta amezidi kuwekewa presha azungumzie mabilioni ambayo ilifichuka kuwa familia yake imewekeza katika nchi za nje.

Kupitia Uchunguzi wa Pandoras Papers, ilifichuka kuwa Kenyatta na familia yake wana akauntyi ambazo zimejaa mabilioni kule Ulaya.

Sasa wakosoaji wake wanasema amevunja maadili kwa kuweka utajiri mkubwa kule nje wakati ambapo Wakenya wanalia na kusaga meno kutokana na kupanda kwa gharama ya kiuchumi.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke