Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

MAGAZETI KENYA: Raila akutana na wajumbe wa Rais wa Dubai

E904419b95ccd294 Raila akutana na wajumbe wa Rais wa Dubai

Wed, 3 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Siasa za uchaguzi wa urais 2022 zinaendelea kushamiri huku ikiarifiwa kinara wa ODM Raila Odinga alisafiri Dubai kupanga kadi zake.

Kuna taarifa pia kuhusu migomo ambayo imekuwa ikishuhudiwa shuleni huku Wizara ya Elimu ikilazimika kuwapa wanafunzi muda wa kuenda mapumziko nyumbani.

1. Standard

Gazeti la Standard linasema wandani wa Rais Uhuru Kenyatta wanapendekeza Peter Kenneth awe mgombea mwenza wa Raila Odinga 2022.

Gazeti hilo linasema hilo limeafikiwa wakati wa kikao kati ya wandani hao na Raila Odinga nchini Dubai alipokuwa amefika kwa kikao cha faragha.

Inaarifiwa wandani wa Rais walimshauri Raila kuwa na mgombea mwenza kutoka Mt Kenya ili iwe rahisi kwake kuukwea Mlima.

Kuna taarifa pia kuhusu pendekezo la maseneta kuwe na sheria ya kuzuia Wakenya kusafiri mpaka nchini Saudi Arabia kufanya kazi.

Hii ni kutokana na visa vingi vya Wakenya kuteseka nchini humu ambavyo vimekuwa vikijiri.

2. People Daily

Gazeti hili limezamia migomo inayoshuhudiwa shule na sasa wizara ya Elimu imeamua wanafunzi waende nyumbani kuanzia Novemba 19 hadi 23 kama njia moja ya kujaribu kutafuta suluhu ya migomo hiyo.

Serikali ilikuwa imeondoa likizo hiyo ya mid term lakini Jumanne Novemba 2 wakapiga abautani.

Hilo linajiri baada ya shule 15 kufungwa baada ya visa vya vurugu na kuchoma madarasa katika kuishinikiza serikali kuruhusu likizo hiyo.

3. The Star

Kuna taarifa kuhusu mwanajeshi wa Uingereza aliyefutwa kazi kwa kuinua nguo ya kipusa katika duka moja.

Inaarifiwa kisa hicho kilifanyika katika duka moja mjini Nanyuki na ilikuwa ni fedheha kwa mwathiriwa na hivyo mwanajeshi huyo akafutwa kazi.

Kuna taarifa pia kuhusu ziara ya DP Ruto katika kaunti ya Kiambu Jumatano Novemba 3 ikiwa ni siku chache tu baada ya Rais Uhuru Kenyatta kuonekana kutoa matamshi ya kumlenga.

Akiongea Oktoba 29 katika eneo la Ruiru, Rais aliwataka Wakenya wasichague 'mwizi' matamshi yamewakera wandani wa DP.

4. Nation

Nation inaangazia faida au hasara kisiasa kwa naibu rais William Ruto akaimua kukigura chama cha Jubilee kabisa.

Ruto amekuwa akijenga nyumba ya UDA baada ya masaibu ndani ya Jubilee baada ya tofauti kuibuka kati ya Rais na DP.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke