Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Likizo imeisha sasa narudi kwa DP Ruto, Didmus Barasa asema

86781386449427eb Likizo imeisha sasa narudi kwa DP Ruto, Didmus Barasa asema

Sun, 6 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Barasa alisema likizo ilikuwa ya kumaliza miradi ya maeneo bunge na itakamilika ndani ya mwezi mmoja

- Alitupilia mbali ripoti kuwa likizo yake ilikuwa ni mikakati ya kuondoka kambi ya kisiasa ya DP Ruto

- Mbunge huyo alisema amekubalina na DP atakabidhiwa wadhifa wa waziri kwenye serikali ya hustlers

- DP Ruto amekuwa akijaribu kupenya eneo la Magharibi katika safari ya kutafuta kura za kuingia Ikulu ifikapo 2022

Mbunge wa Kimilili Didmus Barasa amesema sasa anarejea kwenye siasa tena baada ya likizo ya miezi kadhaa.

Alisema alikuwa amechukua likizo hiyo ili kuchapa kazi ya miradi inayofadhiliwa na pesa za maeneo bunge.

Barasa alipinga ripoti kuwa likizo yake ilikuwa ni mikakati ya kujiondoa kambi ya Naibu Rais William Ruto na mrengo wa Tangtanga.

"Miradi hiyo inakamilika kwa mwezi mmoja ili nirudi kufanya ile siasa yangu ingine. Wengine wakafikiria eti nimechukua likizo kwa sababu nilikuwa nimeondoka kwa chama ya UDA ya william Ruto," alisema Barasa.



Alisema hawezi kujiondoa kambi ya Tangatanga kwani wamepanga karata na DP Ruto ambapo atapewa wadhifa serikalini.

Mimi na William Ruto tuliketi chini kitambo na tukamaliza . . . kuwa akiunda serikali mimi ndio nitakuwa Waziri wa Usalama wa Ndani. Tulipanga hiyo na tukamaliza," alisema Barasa.

Alionya wapinzani wa DP Ruto dhidi ya kuzua machafuko 2022 akisema atakuwa ni waziri na watakiona cha mtema kuni.

"Mimi nitatoa amri kuwa wakamatwe wote wawekwe jela. Hata nikiwa mwembamba hivi amri itaheshimiwa," alisema.

Aliwataka wafuasi wake kumuunga mkono Ruto na azma yake ya kuchukua serikali akisema watanufaika pakubwa.

Mbunge huyo alitangaza kuchukua likizo mwezi Machi mwaka huu lakini hakufichua ni kwa nini atakuwa nyuma ya hema.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke