Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Liberia yaishiwa chakula cha wafungwa

Chakula Wafungwa Liberia yaishiwa chakula cha wafungwa

Thu, 6 Jan 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Magereza yote 15 nchini Liberia wiki hii yameishiwa na chakula cha wafungwa.

Hii imesababisha magereza mawili, ikiwa ni pamoja na Gereza Kuu la Monrovia, kusitisha kwa muda kuwapokea wafungwa wapya muda, maafisa wa magereza wamesema.

Hali hiyo imechangiwa na masuala kadahaa ikiwemo kucheleweshwa kwa fedha za chakula na usimamizi wa magereza.

Lakini mkurugenzi wa magereza, Sainleseh Kwaidah, ameambia BBC siku ya Jumatatu kwamba serikali ilikuwa inafanya kila iwezekanavyo kushughulikia suala hilo.

Alisema baada ya hatua kuchukuliwa magereza mawili ambayo yalikuwa yamesitisha kuwapokea wafungwa yalifunguliwa na vyakula vinapelekwa katika magereza mengine yaliyosalia.

Askari magereza aliiambia BBC kuwa magereza yamefunga milango ili kuzuia kuwaweka watu zaidi hatarini kwa sababu ya uhaba wa chakula. Alisema pia kuna uwezekano kwamba wafungwa wenye hasira wanaweza kupanga njama ya kutoroka jela

Maafisa wa magereza katika siku za hivi majuzi wamekosoa jinsi serikali inavyoshughulikia masuala ya vituo hivyo vya kurekebisha tabia vilivyojaa watu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live