Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Leteni hata G4S Karen wanilinde, DP Ruto asema kuhusu usalama wake

49413f7a588eeb33 Leteni hata G4S Karen wanilinde, DP Ruto asema kuhusu usalama wake

Mon, 30 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Ruto amewataka wandani wake kaucha kulalamika kuhusu kuondolewa kwa walinzi wake kutoka kikosi cha GSUAlisema huenda kuna kazi muhumi ambayo ilipatikana ya kufanywa na GSU hao na ndipo akapewa APs. DP amesema muhimu kwake kwa sasa ni kutafuta mbinu za kubadili mfumo wa uongozi ili kuinua maisha ya Wakenya. Naibu Rais William Ruto amekaribisha kikosi kipya cha walinzi wake kutoka kitengo cha maafisa wa utawala (APs).

Akiongea Nakuru katika eneo bunge la Bahati, DP alisema hakuna haja ya mjadala kuhusu kuondolewa kwa maafisa wa GSU kutoka makao yake Karen an Sugoi.

"Hii mambo ya AP na GSU ni madogo sana. Tafadhali tusipoteze muda mwingi tukiongea iwapo ni GSU au ni AP . . .mimi sina shinda AP wakikuja kulinda mahali naishi. Kama kazi imepatikana wale GSU watumike ili Wakenya wengine wapate usalama, hawa GSU wanafaa kuenda kusaidia hapo," alisema DP Ruto.

Alitaja kinachoendelea kama siasa za mvutano katika serikali huku baadhi ya viongozi wakitaka kuonyesha ndio wenye mamlaka.





"Mimi hata na hao APs wakipatikana kazi ya kuenda kufanya, ikitokea kazi ya muhimu kwa Wakenya ambao wako na matatizo, wanaweza kuniletea hata G4S mimi niko sawa. Tuwache mambo ya watu kujitafutia nani mkubwa, nani mdogo," alisema Ruto.

DP alisema muhimu kwake kwa sasa ni kutafuta mbinu za kubadili mfumo wa uongozi ili kuinua maisha ya Wakenya wanaotatizika katika kutafuta riziki.

"Mimi nataka niwaulize Wakenya wote, ya muhimu tunataka tupange vile tunaweza kubadilisha taifa letu. Kuna wakenya wengi mailioni ambao hawana kazi, hilo ni muhimu kwetu," alisema Ruto.



Wandani wa Ruto wamekuwa wakichemka kisiasa tangu maafisa hao wa GSU waondolewe katika makao yake Karen na Sugoi.

Walisema kuna njama ya kuhujumu DP kwa kuhatarisha usalama wake wakati huu ambapo safari ya kuchapa kampeni za 2022 imeanza.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke