Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Lazima Kitaeleweka: DP Ruto Asema Hakuna Kubembelezana Tena Ndani ya Jubilee

F1c668419c2ca351 Lazima Kitaeleweka: DP Ruto Asema Hakuna Kubembelezana Tena Ndani ya Jubilee

Thu, 25 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- DP alisema joto likizidi ndani ya Jubilee hatakuwa na lingine ila kuondoka na kuimarisha chama cha UDA

- Alisema tatizo ndani ya Jubilee ni kundi la watu ambao wanataka chama hicho kiwe cha kikabila

- DP alikosa kufungua roho kuhusu uhusiano wake na Rais Uhuru Kenyatta akisema muhimu kwa sasa ni katiba inamlinda

Naibu Rais William Ruto kwa mara ya kwanza amefungua roho na kusema yuko tayari kuondoka chama cha Jubilee.

Akiongea kwenye mahojiano na redio Citizen, Ruto alisema ni lazima suluhu lipatikane kwenye mzozo unaokumba Jubilee lakini hali ikibidi basi yuko tayari kuruka nje.

“Mimi nimechaguliwa kwa Jubilee lakini tumekuwa na UDA…tukienda mbele wale ambao wanatusukuma nje ya Jubilee kwa kufukuza watu ndani ya chama ikifika sehemu tutakuwa na mpango mbadala,” alisema Ruto.

Ruto alisema tatizo kubwa ndani ya Jubilee ni kundi la watu ambao wanataka kugeuza chama hicho ili kimilikiwe na jamii fulani.



Alisema wakikosa kupata suluhu ya mzozo ndani ya Jubilee, basi ataruka na kuingia UDA kwenye safari yake ya kuingia Ikulu.

“Ikifika sehemu hatuelewani tutajipanga na UDA kwa sababu ni chama tunajua na sera moja kwa sababu kimekuwa ndani ya Jubilee. Ukitaka kutatua kero za taifa lazima uwe na gari la kitaifa, ikifika tunatumia UDA tutakifanya kiwe chama cha kitaifa," alisema Ruto.

"Kuna watu wanataka kufanya Jubilee chama cha kikabila na wakifanya hivo basi UDA tutakijenga kiwe chama cha kitaifa,” aliongeza.



Ruto alisema viongozi ambao wamekuwa wakiwatimua wengine kutoka Jubilee wana mpango wa kugawanya watu kwa mirengo ya kikabila lakini hawatafaulu.

“Katika mambo haya ya siasa, kuna watu wa fitina, watu ambao muda wao mwingi hawatumii kupanga vile tunaweza kuenda mbele. Hawa wenye kutugawanya, wenye muda wao mwingi ni kufukuza wengine, hawatafaulu,

Kwa sababu Kenya hii, wajinga wamepungua mno wa kuweza kudanganyika ati kwamba wanaweza kubadilisha maisha yao kwa kugawanywa ati kila mtu aende kwa kabila yake. Wakenya wamewaona kutoka mbali, ya kwamba mipango yao ni ya kibinafsi,”alisema.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke