Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kutana na mwanamke mwenye sehemu za siri mbili na mifuko miwili ya uzazi

83b921fb014335d8 Kutana na mwanamke mwenye sehemu za siri mbili na mifuko miwili ya uzazi

Sun, 10 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mwanaharakati wa afya ya uzazi nchini Ghana kwa jina Elizabeth Amoaa, amesimulia namna aligundua ana mifuko miwili ya uzazi, na sehemu nyeti mbili za uke.

Amoaa pia alifichua alikuwa akijidharau akidhania kwamba amelaniwa kabla ya kutambua hali yake ncgini Ujerumani Kutokea wakati huo alijikubali na kusema kuwa anajipenda jinsi alivyo.

Elizabeth Amoaa, ambaye ni balozi wa afya ya uzazi, alisimulia hali yake na namna aligundua ana mifuko miwili ya uzazi, na sehemu nyeti mbili za uke .

Kulingana naye, aligundua hali yake miaka mitano baada ya kujifungua binti yake.

Amoaa pia alifichua alikuwa akijidharau akidhania kwamba amelaniwa.

Mwaka 2015, Amoaa aligunduliwa kuwa na tatizo kwa jina la kisayansi ''double uterus,'' hali ambayo hutokea wakati mtoto anakua tumboni, hii ni wakati tubu mbili za mfuko wa uzazi zinagawana na kuwa mbili kulingana na ripoti ya kliniki ya Mayo.

Kwa mujibu wa Health.com,chupa mbili za uzazi zinaweza kuwa na mlango mmoja wa uzazi ama kutengana na hivyo mwanamke kuwa na mifuko miwili ya uzazi na uke mbili.

Akizungumza katika mahojiano na GTV Breakfast kwenye GBC, alisimulia safari yake ya ujauzito.

Alielezea namna madakatari walidhani kwamba mimba yake ilijitunga kwenye ukuta wa uterasi.

Madaktari walimshauri kuavya mimba hiyo lakini alikataa na baadaye kuzaa mtoto wa kike kwa jina Rashley.

''Binti yangu alizaliwa kabla ya wakati. Kuna mengi yaliyotokea katika miaka 20-30 ya maisha yangu.Kitambo nilifikiria nimelaaniwa lakini leo nikiwa hapa ni baraka kuliko laana," alisema.

Amoaa alisema hali yake ilimupa maumivu sana wakati wa ujauzito wake lakini alipogundua ana mifuko miwili ya uzazi, alifunguka macho na kugundua mbona madaktari walishindwa kutambua hali hiyo.

Hii hapa video ya mahojiano hayo

Amoaa aliangaziwa na TUKO.co.ke akizungumzia uchungu aliopitia kabla ya kugundua hali yake.

"Hedhi yangu kila wakati ilikuwa nzito sana. Nilikuwa nikilalamika sana juu ya maumivu ya tumbo lakini mama yangu aliponipeleka hospitalini madaktari waliendelea kunipa dawa wakisema tu nilikuwa na upungufu wa damu au nilikuwa na maambukizi ya chachu," alisimulia.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke