Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kuna panya ndani ya Jubilee, tutawamaliza na nyumba kusalia salama

123eb9be4ef8b33a Kuna panya ndani ya Jubilee, tutawamaliza na nyumba kusalia salama

Thu, 17 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Nyoro alisema kuna panya ambao wanazurura katika nyumba ya Jubilee lakini chuma chao kiko motoniAlisema hawawezi kubomoa nyumba yote au kuichoma ila watawafurusha ili nyumba isalie salamaMawimbi yamekuwa yakiyumbisha Jubilee huku wengi wakiamini chama hicho kitakuwa hofu ifikapo 2022Gavana wa Kiambu James Nyoro amesema chama cha Jubilee kitastahimili mawimbi yaliyopo na kuvuma hata baada ya 2022.

Alisema masaibu yanayoshuhudiwa kwa sasa ndani ya Jubilee yameletwa na watu ambao alisema ni wakaidi wa chama.

Alisema hao ni panya na wanachama wengine hawatakubali nyumba kubomolewa kwa sababu ya panya hao.

"Chama cha Jubilee kitakuwepo hata baada ya 2022. Kama una nyumba na kuna panya, hutachoma nyumba yote.Unatimua panya na kubakia katika nyumba hiyo. Jubilee itakuwepo hata baada ya 2022," alisema Nyoro.



Gavana huyo alikuwa akizungumza siku chache tu baada ya wenzake wa Nakuru na Kirinyaga Ann Waiguru na Lee Kinyanjui kusema mageuzi yanatakikana chamani.

Wawili hao walisema chama kimepatwa na masaibu na kuna haja ya kubadili uongozi ambao umekuwepo la sivyo chama kizame na kusahaulika.

Waiguru alisema mambo yamebadilika na kuna haja ya uongozi wa chama kukubali kuwaleta watu wenye mtazamo tofauti ili kufufua sifa ya Jubilee.

Aidha Nyoro alisema bado ni mapema kwa Wakenya kutabiri ni nani atawika kwenye uchaguzi wa urais wa 2022.

Alisema kulingana na historia ya siasa za Kenya, wagombea wa urais hujulikana vizuri miezi mitatu kabla ya kura ya kiti hicho kupigwa.

"Unaweza kuangalia marais waliopita. Nafikiri bado ni mapema kutabiri. Tuna na mwaka mmoja na miezi minne. Sasa tuko mpaka na magavana ambao wanataka kuwania urais," alisema Nyoro.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke